Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuunga mkono Hotuba ya Kambi ya Upinzani Bungeni. Naomba Serikali ione haja ya kuwaokoa Watanzania wanaoishi Wilaya ya Kilombero, Jimbo la Mlimba ambako jimbo zima pamoja na kuwa na miundombinu mibovu lakini hakuna huduma ya uhakika ya Mahakama. Hivyo kupelekea watu wengi kukaa mahabusu kwa kukosa usafiri ama mashahidi kushindwa kufika mahakamani kutoa ushahidi, zaidi ya kilometa 260 hadi Mahakama ya Wilaya iliyopo Ifakara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu, naomba Mheshimiwa Waziri atembelee Jimbo la Mlimba; pili, tupatiwe mahakama Jimbo la Mlimba; na tatu Mahakimu waajiriwe ili haki zipatikane.