Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuishauri Serikali kupitia upya sheria mbalimbali, naomba Serikali itafute utaratibu wa kila Tarafa nchini kuwa na Mahakama za Mwanzo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wa kupata wazee wa Mahakama uboreshwe. Hivi sasa wazee wengi wa Mahakama wanakaa muda mrefu bila kuteuliwa kwa kuzingatia jinsia na kutoka Kata au Tarafa kulingana na idadi yao, hata hivyo uteuzi haushirikishi Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mabaraza ya Ardhi baadhi yake yamejihusisha na rushwa kiasi kwamba wapokea huduma toka Mabaraza mbalimbali nchini yanakosa imani.
Kwa sasa kuna haja ya ufafanuzi wa Wizara kuhusu masuala mbalimbali ya wananchi kufahamu utaratibu wa kupata haki zao mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Wakuu wa Wilaya ndiyo Wenyeviti wa Kamati ya Maadili ya Mahakama. Kuna haja ya kuwa na ratiba ya vikao vya Kamati hiyo muhimu kwa ustawi wa Mahakama nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siku ya Maadhimisho ya Mahakama nchini itumike kuwa siku ya wapokea huduma kutoa mawazo yao kuhusu huduma hiyo ili Watendaji wa Mahakama waweze kujijua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo wa malipo ya Wazee wa Mahakama utazamwe ili kuleta tija, kwa sasa wazee wengi wanalalamikiwa kujihusisha na rushwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuwe na kipindi cha kuwahabarisha umma kuhusu huduma ya Wasaidizi wa Kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali isaidie kutoa fedha za ujenzi wa jengo la Mahakama ya Wilaya ya Mbulu na Jengo la nyumba ya Hakimu wa Wilaya. Kwa sasa majengo yaliyoko ni chakavu sana, hayafai kwa matumizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Wilaya ya Mbulu yenye Kata thelathini na tano ina Mahakama moja ya Wilaya na Mahakama za Mwanzo tatu lakini Mahakama za Mwanzo haina Mahakimu wa kutosha na kesi nyingi huchelewa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naomba Waziri mwenye dhamana afanye ziara Wilayani Mbulu na kuona changamoto ya Wizara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante.