Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Twahir Awesu Mohammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mkoani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. TWAHIR AWESU MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia na kuwezesha kupata fursa hii muhimu ya kutoa mchango wangu huu katika hoja hii iliyopo mbele yenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haki za binadamu, tumekuwa na tabia kwa Serikali yetu hii tukufu kuweka maneno kwenye makaratasi mazuri yenye kuonesha kwamba nchi inafuata taratibu nzuri za kisheria suala zima la utoaji na utekelezaji wa haki za binadamu wakati haki hiyo haipo na haipatikani badala yake Serikali na vyombo vyake vya dola vinatumia nguvu kupita uwezo kwa kuwakandamiza na kuwanyanyasa raia zake kuwekwa magerezani na kuwapa vifungo kwa makosa ya kuwabambikiza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na watuhumiwa wa makosa ya ugaidi zaidi ya miaka minne sasa Watanzania wenzetu wamo wanateseka na kufanyiwa vitendo vya kinyama na kiudhalilishaji wako mbali na familia zao. Kesi hadi leo inaelezwa ushahidi haujakamilika, naiomba Serikali kwanza itambue hapa duniani tunapita, iache kutesa raia zake, basi kama wanahatia ni vyema wakahukumiwa, wakapewa adhabu kulingana na ukubwa wa makosa yao na kama makosa hayakukidhi wakaachiwa huru wakarudi na kuishi na familia zao ambazo hivi sasa zinateseka sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la katiba mpya, suala hili sasa si suala rahisi tena kutekeleza ni dhahiri Serikali halimo kabisa katika mpango wake wa utekelezaji wake, pamoja na Watanzania kuhitaji sana suala hili. Ni vyema kwa Serikali kuzingatia na kusikiliza maoni na matakwa ya wananchi wake kuepusha nchi yetu kuingia katika kutoelewana kitu ambacho kinaweza kuleta mgawanyiko mkubwa, utakaopelekea Taifa kusambaratika na kugombana wenyewe kwa wenyewe. Naiomba Serikali ikae na ilifikirie jambo hili kwa umakini mkubwa ili thamani ya kazi na michango waliyotoa Watanzania ionekane umuhimu wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.