Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa wakati anazungumza Bungeni akijibu swali la Kiongozi wa Upinzani, alisema Serikali yetu hii tuiamini sana ifanye uchunguzi wa mambo haya ya utekaji na utesaji na sisi humu ndani ukiuliza nani haiamini hii Serikali hayupo atakayetokea. Kwa sababu Serikali hii ni yetu sote ndiyo maana tuko hapa tunaisimamia Serikali, tuko hapa tunaishauri Serikali, lakini Serikali inayotaka kuaminika ni lazima iwe wazi. Hivi kwa mfano mtu aliyetaka kumpiga risasi Mheshimiwa Nape hajulikani, Serikali haimjui, kama inamjua basi ijitenge naye, kama haimjui iseme, lakini tunavyojua Serikali inamjua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna makosa ya kijinai yametendwa katika nchi hii na watendaji wa Serikali. Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ameingia kwenye chumba cha habari akitumia silaha, kwa mujibu wa sheria zilizopo ule ni unyang’anyi, wizi wa nguvu. Amekwenda kupora CD za chumba cha habari. Kamera zimeonesha, Tume ya Mheshimiwa Nape Nnauye imeripoti. Ripoti ya Tume ya Mheshimiwa Nnauye imeundwa na waandishi wa habari na imekuwa submitted kwa Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu anayetenda jinai, DPP yuko pale, moja ya majukumu yake ni kuendesha kesi za jinai mahakamani, lakini pia kuangalia ni nani anayetenda jinai kuagiza DCI wafanye uchunguzi, hiyo ndiyo kazi ya DPP. Sasa DPP yupo amenyamaza, polisi wapo wamenyamaza. Mtu anatumia jina ambalo sio lake, ametenda makosa mengine yenye adhabu ya zaidi ya miaka 30 gerezani. Watu wamekwenda mpaka Kolomije, wamekwenda nyumbani kwao kijijini kwake wamezungumza na mama yake, vyombo vya habari vimefika huko, Waziri Mkuu anasema tuiamini Serikali, tunaiamini kweli lakini Serikali lazima iwe wazi iache double standards. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watumishi wa umma kwenye nchi hii wamefukuzwa kazi wengine wameshtakiwa wamefungwa lakini mtu mmoja anaitwa Paul Makonda jina lake Daudi Bashite anaachwa kwa sababu gani, who is Makonda? Mtu anaingia kwenye chumba cha habari akiwa na silaha za moto na polisi, who is Makonda? Halafu Serikali inasema iaminike, waandishi wa habari wanafanya kazi kwenye mazingira magumu halafu Waziri wa Habari ananyamaza, inasikitisha. Waziri wa Habari ananyamaza, ameona waandishi wa habari wananyanyasika kwenye nchi hii anatetea uhalifu halafu anasema tuamini Serikali, tunaaminije? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna makosa zaidi ya nane wanasheria wanasema. Rais wa Chama cha Wanasheria yuko humu ndani, TLS haichukui hatua dhidi ya Makonda, Tume ya Haki za Binadamu haichukui hatua dhidi ya Makonda halafu mnasema Serikali tuiamini. Bunge limenyamaza linapigwa pini, linapigwa kufuli lisimzungumzie Makonda, jamani, halafu mnasema tuamini Serikali, Serikali inaaminikaje ikiwa imejifunika kwenye blanketi. Kutoa silaha hadharani ni kosa la jinai. Leo Kamishna Siro amesema ni kosa la jinai, Mheshimiwa Nape ametolewa silaha hadharani. Juzi watu wametoa silaha hadharani, aliyetoa silaha Mheshimiwa Nape anamjua, dunia inamjua, vyombo vya habari vinamjua, waandishi wa habari ndio waliozuia…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya Kambi ya Upinzani, nashukuru sana.