Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

Hon. Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Katiba na Sheria

MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa dakika chache nilizopata, lakini namwomba Mwenyezi Mungu niweze kuzitendea vyema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu napenda kujielekeza kwenye suala zima la usafirishaji wa binadamu ambao ni Watanzania kwenda nchi za nje kufanya kazi na wengi wao wamekuwa wakiuawa na clips zinatumwa hapa nchini, zinazagaa kwenye mitandao ya kijamii, sisi kama Wabunge tunaona, Serikali imekaa kimya haisemi jambo lolote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali hii ni hatari kwa sababu hawa wanaofanya biashara hii ya kusafirisha binadamu kwa maana ya human trafficking na kuwapeleka huko wanakwenda kuuawa kinyama, kwa nini Serikali haifanyi msako maalum wa kuhakikisha inawakamata? Vijana wetu tena vijana wa kike wanakwenda huko wanafanyiwa unyama lakini Serikali imekaa kimya. Tunataka tamko leo litoke, ni hatua gani zimechukuliwa kubainisha watu wanaosafirisha wasichana wa Kitanzania bila ridhaa ama kwa ridhaa lakini kwa udanganyifu. Wanakwenda kwa wazazi wanawahonga dola 200, 300 wanawaambia kijana wako anakwenda huko atafanya kazi nzuri supermarket, wapi, akifika kule anadhalilika anauawa, Serikali inasemaji juu ya hili? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo napenda kulizungumzia ni conflict of laws. Nchi yetu ina tabaka za watu mbalimbali, kuna mila na desturi mbalimbali. Sheria zetu zimeingia kwenye mgongano, tuna Sheria ya Mirathi lakini pia tuna Sheria ya Ndoa, tunayo Islamic Restatement Act lakini pia tunayo Sheria ya Kimila ambayo ni Customary Declaration Order ya mwaka 1963.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi sheria zinakinzana, kuna sheria ambayo inamtambua mtoto ni kuanzia umri wa miaka 21 lakini kuna sheria inayosema mtoto mwisho wake itakuwa ni miaka 18, lakini kuna sheria za Kiislamu zinazosema mtoto mwisho wake ni pale anapobalehe. Sasa linapokuja suala la mtoto aolewe ama aozeshwe kwenye umri gani ama aoe kwenye umri gani kuna mwingiliano wa mila, desturi, dini na sheria. Je, mambo haya tunakwenda nayo vipi? Ni lazima mijadala ya kina ifanyike ili kuhakikisha kwamba pande zote zinabaki bila dukuduku. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi siungi mkono ndoa za utotoni, naunga mkono wanaopendekeza watoto waolewe kuanzia umri wa miaka 18. Hata hivyo, kuna watoto ambao na wenyewe wanaingia kwenye mapenzi kabla ya umri suala ambalo linapelekea ubebaji wa mimba. Sasa mtoto yule alivyopata mimba kwenye umri wa miaka 13, 14 ni mzazi gani atakayekubali kuona mtoto wake mwenye umri huo mdogo anakaa nyumbani na anazalishwa, hapohapo sheria zetu haziwaruhusu watoto hao kuendelea na shule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tukubaliane, kama tutaamua mtoto aanzie umri wa miaka 18 aweze kuoa na kuolewa, je, mtoto anayepata ujauzito kabla ya miaka hiyo status yake itakuwaje? Kama tutakubaliana miaka 18 basi kuwe kuna exception, kama atapewa ujauzito kabla ya hapo aruhusiwe kuozeshwa kwa sababu kuna watu ambao mila zao kukaa na binti nyumbani mama yake mzazi anapata ujauzito na mtoto anapata ujauzito ni matusi. Naomba hili lifanyiwe kazi kwa namna ya kipekee. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda kuzungumzia suala moja, tunayo Sheria ya Probate and Administration of Estate Act ya Tanzania ambayo inaunda Waqf Commission. Wenzetu wa Zanzibar tayari wana Waqf Commission na watu ambao wanataka mali zao zigawanywe kwa mtindo huo wanakwenda kwenye Waqf Commission wanapeleka mapendekezo yao na yanafanyiwa kazi. Kwa upande wetu wa Tanzania Bara tume hii ipo kwenye sheria lakini haijawahi kuundwa toka uhuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka majibu kutoka kwa Mheshimiwa Waziri, ni lini Serikali itaunda Waqf Commission kwa upande wa Tanzania Bara ili wale ambao wanajisikia kupeleka mali zao pale ambazo zitakuja kusaidia vizazi vinavyokuja basi waweze kuzingatiwa na waweze kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, umuhimu wa hili ni nini? BAKWATA imekuwa na malalamiko mengi sana, watu wengi hapa nchini hawana imani na BAKWATA hususan Waislam wengi hawana imani na BAKWATA. BAKWATA wanauza mali za Waislam, BAKWATA wanaingia kwenye migogoro wamewauzia akina Yussuf Manji mali za Waislam, kesi, vita, ngumi kila siku. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini sasa msitengeneze hii Waqf Commission ambayo itatoa sasa mali hizi ambazo zinawekwa kwenye mikono ya watu ambao kwa kiasi fulani hawaaminiki ziweze kuwa kwenye mfumo wa Serikali ili…
T A A R I F A....
MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namsikitikia sana Mbunge mwenzangu aliyesimama, kama ni Mtanzania ambaye anafuatilia vyombo vya habari na anafuatilia habari za kila siku katika nchi hii hawezi kuhoji BAKWATA kwamba haikubaliki na kundi kubwa la Waislam Tanzania. Kwa hiyo, hilo ni jibu ambalo linamtosha kama halijatosha aje nitampa research na mifano ya kesi ambazo BAKWATA wameuza mali za Waislam, kitu ambacho kinapelekea vita nchi hii.
Kwa hiyo, napendekeza kabisa kwamba Waqf Commission iundwe kama ilivyo Zanzibar ili hawa waporaji ambao wamejificha kwa mgongo wa BAKWATA suala hilo liweze kwisha na lipatiwe muafaka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kugusia suala zima la migogoro ya kazi katika chombo chetu cha Commission of Mediation and Arbitration. Chombo kile tumekianzisha ili kiweze kupunguza mrundikano wa kesi za labour hususan katika mahakama zetu kuu. Hata hivyo, nasikitika kusema kwamba, majengo yake hayatoshi ku- accommodate wateja wanaokwenda pale. Ukienda pale unakuta makundi ya watu yamekaa kwenye vyumba vidogovidogo, kelele, hata wale wanaosikiliza mashauri hawawezi kuelewana, joto, giza, mrundikano wa watu, mpaka watu wengine wanafanya kupangiwa …
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.