Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ruzuku kwa wananchi wanaokuza miche ya miti na wanaopanda miti Mafinga. Wananchi wa Mafinga na Mufindi kwa ujumla wamekuwa hodari katika kupanda miti na kutunza mazingira kwa ujumla. Hata hivyo, wananchi hawa kwa kiasi kikubwa wameachwa kama yatima hasa kutoka katika Wizara hii. Angalau Maliasili na Utalii kupitia Shamba la Sao Hill wamekuwa wakitoa mbegu (miche) kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuunga mkono juhudi za wananchi wa Mafinga na Mufindi kwa ujumla, Wizara hii ije na mpango wa kutoa ruzuku kwa wananchi wanaojishughulisha na upandaji wa miti. Suala hili linaweza kuwa kichocheo kwa wananchi wa maeneo mengine hapa nchini kuona umuhimu sio tu wa kupanda miti kwa mazoea kama ilivyo hivi sasa. Ruzuku kwa wakulima/wananchi wanaopanda miti itakuwa kichocheo kikubwa cha lengo la kuhakikisha nchi yetu inakuwa ya kijani (ukurasa wa tisa (9)).
Mheshimiwa Mwenyekiti, Baraza la Usimamizi wa Mazingira; kutokana na ongezeko la majukumu, ni wazi kuwa NEMC imezidiwa kutokana na uhaba wa watumishi. Ni kwa sababu hiyo ndiyo maana hata elimu ya mazingira kwa umma imekuwa haifanyiki ipasavyo. Naishauri Serikali ione haja sasa ya kuongeza watumishi katika ofisi hii muhimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upandaji miti bila kuitunza ni bure; nchi yetu imekuwa na kampeni kubwa ya upandaji miti, tukiwa realistic ni asilimia ndogo mno ya miti iliyopandwa ambayo inaendelea kuwepo. Nashauri Wizara ibadilishe mikakati ili tusiishie tu kuwa tunapanda miti bila kuitunza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.