Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mabadiliko ya tabianchi; pamoja na juhudi za Serikali katika kulinda mazingira hususan pembezoni mwa fukwe za bahari na pembezoni mwa maziwa yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto katika Ziwa Tanganyika; naomba Serikali iangalie upya ujenzi wa hoteli na nyumba za kuishi pembezoni mwa Ziwa Tanganyika, je, wanafuata taratibu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, wavuvi; kuna baadhi ya wavuvi ambao sio wazalendo ambao wanatumia baruti na nguvu ambazo hazifai katika vyanzo vya maji mpaka sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tafiti za gesi zinazoendelea baharini, ni jambo jema Serikali kuendelea kuruhusu uchunguzi au tafiti zinazoendelea kufanywa na wawekezaji katika Bahari ya Hindi ili wagundue ni wapi na gesi ipo kiasi gani katika bahari. Wawekezaji wana vifaa vyao na sio Watanzania/uzalendo kuhusika? Je, Serikali ina uhakika gani tafiti zinazofanywa katika bahari juu ya uvumbuzi wa gesi kwamba haiathiri mazingira chini ya bahari? Je, Serikali ina mkakati gani ili inunue vifaa vya uchunguzi kujua wawekezaji hao hawaathiri mazingira baharini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, malalamiko ya wananchi wanaotoa taarifa kwa polisi kuhusu viwanda feki vinavyotuhumiwa kuharibu mazingira, mifuko ya plastiki, ukataji wa miti ya asili kiholela, wino – viwanda, viwanda vya viroba kiholela, uvuvi haramu. Wananchi ni wazalendo na mazingira yao lakini wanapoisaidia Serikali kuwataarifu, Serikali na hawa wanaoharibu mazingira wamekuwa wakitajwa, je, Wizara yako inatoa tamko gani? Wananchi wakiwa kimya bila kutoa taarifa kuhusu uharibifu huu mazingira mnategemea nini kama sio jangwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wachina wanaojenga barabara waharibifu wa vyanzo vya maji Mkoa wa Katavi; Mto Kuchoma Wilayani Mpanda umekauka kutokana na matumizi makubwa ya maji yanayotumiwa na mkandarasi huyu. Serikali inatoa tamko gani ili kunusuru mto huu kwa matumizi ya wananchi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mto Katuma pamoja na banio za umwagiliaji; pamoja na Serikali kusimamisha ujenzi wa vibanio kiholela katika Mkoa wa Katavi ambao kwa sasa wakulima wanapata maji, urasimu wa kupata vibali ili kujenga vibao vya kisasa na vinavyofuata utaratibu wa kulinda vyanzo vya maji mkoa mzima kuna vibanio sio zaidi ya vitatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itapunguza urasimu huu wa kupata vibali halali vya mabanio unaofanywa na baadhi ya watendaji au ni utaratibu unaofanywa na Wizara husika? Hii inaleta usumbufu mkubwa, Serikali inasema nini katika hili, waathirika wakubwa wakiwa wakulima hususan Mkoa wa Katavi. Jambo hili liangaliwe upya.