Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehemu waja wake wote pasipo ubaguzi. Nikushukuru wewe kwa kunipa nafasi hii muhimu na mimi nichangie mada iliyopo Mezani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze mchango wangu kwa kuperuzi ukurasa wa 49 wa kitabu cha Waziri kuhusu fedha za Mfuko wa Maendeleo wa Jimbo. Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo upo kisheria, Sheria Na. 16 ya mwaka 2009, pamoja na nia njema ya Serikali ya Muungano wa Tanzania kuchochea maendeleo ya Jimbo, Mfuko huu bado zipo changamoto ambazo zinahitaji ufumbuzi wa kina kustawisha utekelezaji wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utoaji wa fedha umekuwa adha kwa majimbo ya Zanzibar – mara nyingi kama sio zote, majimbo ya Zanzibar huchelewa kupata fedha hii wakati majimbo ya bara wanapata mapema sana. Kwa mfumo huu na ucheleweshaji huu unasababisha kudumaza maendeleo yanayokusudiwa; Zanzibar tunapata fedha hizi ambapo vitu vimepanda, thamani ya fedha yetu imeshuka. Kwa muktadha huo, naomba nipate sababu ya kucheleweshwa kwa fedha hii kwa Zanzibar. Pia nipendekeze kwa kuwa Jamhuri ya Muungano ni moja na Bunge moja, fedha hii itolewe kwa muda muafaka kwa Wabunge wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine kuhusu Mfuko huu, hauongezeki tangu ulipoanzishwa wakati mahitaji yanakua, kila siku watu wanaongezeka. Naomba Serikali ipitie upya Mfuko huu ili ione mahitaji kwa sasa na kuongeza Mfuko huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uwiano wa ajira za Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar. Pamoja na makubaliano yaliyopo Zanzibar 21% na Bara 79%, lakini bado utekelezaji wake hauko wazi na umebakia kwenye makaratasi tu. Naomba uwekwe wazi kwa vitendo.