Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuwa ni desturi wawekezaji wa madini kupewa Mining License katika maeneo ya hifadhi ya misitu. Katika maeneo mengi wanayopewa hufyeka miti ovyo na kuchimba humo na kuharibu kabisa mazingira ya asili ya eneo hilo. Mfano katika Mkoa wa Geita maeneo ambayo yalikuwa na misitu mikubwa yote yamefyekwa na sasa ni jangwa. Aidha, sheria inawataka kufanya recovery (reforestation) baada ya kumaliza kazi (exit plan).
Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe kwamba katika kipindi ambacho mgodi unaendelea kuleta madhara ya uharibifu huwapata wenyeji. Hivyo, madhara hayo huwezi kuyafidia baada ya mika 20 kwa kupanda miti. Maoni yangu ni kuwa:-
(i) Serikali ianzishe Sheria mpya ambapo mmiliki wa mgodi awajibike kutunza Maliasili zote katika eneo lake la license tangu siku ya kwanza ya kutoka, kwani kwa utaratibu hivi sasa mwenye license huangalia madini pekee (ardhini) na kutowajibika na uharibifu unaofanywa na wananchi katika eneo lake, isipokuwa kama watagusa madini. Mfano mzuri Geita Mjini msitu wote katika eneo la GGM umekwisha.
(ii) Serikali ianzishe mfumo maalum (Nature Resources Extract Fund) kama ulivyo Norway, USA na nchi za Kiarabu, maalum kwa ajili ya kuja kushughulika na rehabilitation kwenye maeneo yote yanayoathirika na miradi ya wawekezaji ambayo huvuruga kabisa mfumo wa maisha ya watu na wanyama wa eneo husika. Hivyo mfuko huo utasaidia kutoa elimu, majanga ya asili na kurudisha maisha yanayohusika kama kawaida baada ya miradi kukoma.