Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza kazi nzuri inayofanywa na Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri katika Wizara hii. Pamoja na pongezi hizo nina mchango katika maeneo yafuatayo:-
Hifadhi ya Mazingira ya Bahari; ni wazi kuwa jitihada zetu za kuzuia uvuvi haramu ambao huharibu mazingira ya bahari na kuathiri maisha ya viumbe baharini bado hatujafanikiwa vya kutosha. Bado kuna matukio mengi ya uvuvi haramu ambayo yamekuwa yakitokea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na sababu nyingine zinazochochea uvuvi huu ni kukosa nyenzo za kisasa za kuvua kwenye bahari kuu. Huko awali tulikuwa na mradi wa MACEMP ambao ulikuwa unasaidia kukabiliana na changamoto hizi. Katika mradi huu wakazi wa pwani waliwezeshwa kutegemea shughuli nyingine na kupunguza utegemezi wa bahari. Kwa kuwa bado wananchi wa pwani wanaendelea kukumbana na changamoto hizi ni vema Mradi huu ukaendelea hata kwa kutumia fedha zetu za ndani baada ya kukamilika kwa muda wa mradi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mto Ruvuma; tabia ya kubadilika uelekeo wa Mto Ruvuma na matawi yake usiachwe bila kuwa na stadi ya kutosha. Naomba Serikali ichukue hatua za makusudi ili kudhibiti madhara yanayoweza kujitokeza hapo baadaye. ‘stadi’ hiyo ifanywe tangu unakoanzia na unakoingia Mto Ruvuma.