Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naipongeza hotuba ya Kambi ya Upinzani ya pamoja na Serikali kufanya warsha, makongamano na mjadala mbalimbali ya kushughulikia kero za Muungano lakini kwa kuwa Muungano unahusu binadamu (watu) lazima kero zitaendelea kupatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika moja ya kero ya Muungano ni kitendo cha kupeleka Wanajeshi, Polisi, Mgambo, pamoja na silaha nzito na nyepesi wakati wa uchaguzi, hili jambo ni kero kwa wale wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waishio Zanzibar, nahoji je, hata Visiwa vilivyopo katika Ziwa Victoria navyo vinapelekewa vikosi na silaha kama Zanzibar?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri hadi kufikia hapo, wanaona ni kero na vitisho. Naishauri Serikali iache kupeleka vikosi na silaha toka Bara na kupeleka Zanzibar ili kuifanya demokrasia ya Tanzania ichukue mkondo wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bidhaa zinazoingia Zanzibar, zote zinalipwa kodi lakini cha kushangaza mwananchi yoyote akinunua hizo bidhaa na kuja nazo Tanzania Bara anatakiwa alipe upya ushuru wa forodha kupitia TRA. Naishauri Serikali kulipia mara mbili ushuru ni udidimizaji ushuru, bidhaa zinazoingia Bara zisilipishwe forodha mara mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mazingira yanazingatia uwanda mpana na pia baadhi ya watu hawafahamu mazingira ni nini? mfano katika Jiji langu la Tanga yapo mambo mengi ya utunzaji wa mazingira mfano, open space (Viwanja vya wazi, viwanja vya michezo, Bustani za kupumzikia lakini mengi ya hayo maeneo yanasimamiwa na Halmashauri zetu, lakini sasa yameporwa na itikadi za vyama vya siasa. Naishauri Serikali ifute usia wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamini William Mkapa kuwa viwanja vyote vya michezo , viwanja vya wazi na bustani zimilikiwe na Halmashauri (TAMISEMI).
Mheshimiwa Mwenyekiti, Maafisa Mipango Miji maeneo mengi katika Halmashauri zetu wanashindwa kupanga miji yetu, wanamilikisha viwanja vya wazi, michezo na bustani kwa kupima viwanja na kuwauzia kwa uroho wa kupata fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali Afisa Mipango Miji/Ardhi atakayefanya umilikishaji ardhi hovyo awajibishwe mara moja.