Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MENDRARD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri kuhusu uharibifu wa mazingira. Binadamu wanaharibu sana mazingira kutokana na kilimo cha mabondeni. Nashauri, Serikali iendeleze kilimo cha umwagiliaji ili kuepusha kilimo cha mabondeni
Mheshimiwa Mwenyekiti, ufugaji mbovu wa mifugo kwa mfano ng’ombe. Ushauri wangu ni kwamba, wafugaji
waelimishwe ili kufuga ng’ombe wachache kuepusha uharibifu wa mazingira na kusababisha mito kukauka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, carbon trade, naomba Serikali kuhamasisha wananchi kupanda miti kwa wingi katika maeneo mbalimbali ya nchi ili kulinda mazingira pia ni biashara ya hewa ukaa ambayo itasaidia sana kuinua uchumi wa nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu, wananchi wapewe elimu ya kutosha kuhusiana na utunzaji wa mazingira, kwa mfano waepuke ukataji miti ovyo, kuchoma mkaa na ukataji wa kuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.