Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Twahir Awesu Mohammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mkoani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. TWAHIR AWESU MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uzima na kunifanyia wepesi na fursa ya kupata nafasi ya kutoa mchango wangu huu kwa njia ya maandishi katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakiri na kuamini suala la Muungano wetu ni la msingi na la umuhimu sana kwa faida ya washirika wa nchi zote mbili za Muungano wetu. Nakubali wananchi wa nchi zote mbili hawalalamikii kuwepo kwa Muungano, lawama zinakuja ni namna gani ifanyike kuuboresha na kuondoa malalamiko yaliyopo ikiwa ni pamoja na zinazoonekana kama ni kero kubwa kwa Muungano wenyewe
Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa vikao viwe vimekaliwa na watu wa pande zote mbili kukubaliana tatizo siyo vikao kukaliwa, tatizo kubwa hapa siyo kukaliwa kwa vikao tatizo ni kupatiwa ufumbuzi kero zile zilizolalamikiwa kutatuliwa lakini pia tatizo hapa ni kukaliwa vikao lakini wakimaliza vikao wahusika kukaa kimya wananchi wanaolalamika hawapewi taarifa za yale yaliyoamuliwa na kukubaliana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF III) una manufaa na faida kwa wananchi wa pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, uendelezwe na uimarishwe. Nashauri ili makusudi yaliyoazimiwa yawafikie walengwa halisi na wale waliokusudiwa ni vyema mfuko ukabadilisha utaratibu wa kuifikia jamii inayohusika kwa kuwatumia viongozi wa kijamii wenyewe kuliko kuwatumia viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiwemo Masheikh. Nashauri kwa nia njema kabisa viongozi wa mfuko wawatumie viongozi wa NGO’s ili wananchi wayafaidi vyema matunda halisi ya mfuko huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.