Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kwanza kabisa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya na kunipa uwezo wa kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuwapongeza Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais kwa kazi nzuri sana ya kuendeleza uongozi bora katika nyetu. Ni mfano wa kuigwa katika uongozi wake kwa kuwa mfuatiliaji mzuri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niwapongeze Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri kwa kuonesha nia na njia ya kuboresha masuala ya mazingira kwa ujumla na pia kuonesha na kutekeleza vyema uboreshaji wa Muungano wetu, kuendelea kuboresha kwa kutatua changamoto za Muungano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri katika masuala mawili muhimu na yote yanalenga mazingira. Kwanza napongeza uzinduzi wa Mfuko wa Mazingira Kitaifa ulioanzishwa 2004, tumechelewa lakini tunasema unapoamka ndipo pamekucha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri Mfuko huu tuangalie namna ya kupatia vyanzo vya kudumu ili uwe endelevu na malengo yake yatimie. Suala la athari za Mazingira linajulikana na hakuna hatua ya uhakika inachukuliwa, tunabaki kulalamika wote bila kuchukua hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuhitaji Sheria mpya, zilizopo zinakidhi na pia urasimu wa kubadilisha Sheria na Kanuni zake itachukua muda. Tuhakikishe tunafuata sheria zilizopo, nashauri agizo litolewe na mmoja kati ya vigezo kwa kiongozi yoyote na mtumishi wa Serikali katika ufanisi wa kazi yake iwe masuala ya mazingira, tuzo itolewe kwa kila ngazi kwa taasisi na binafsi katika usimamizi wa mazingira na sheria zake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuongelee na kuhakikisha kuwa Bunge lipitishe sheria ya kuweza kupata vyanzo vya kudumu katika Mfuko wa Taifa wa Mazingira. Pia napendekeza kuondoa kodi katika uagizaji wa majiko yote yanayotumia gesi (LPA) au majiko banifu. Hii itafanya kushuka bei ya gesi na majiko yake na kupunguza uharibifu wa misitu kwa asilimia mbili au tatu. Pia tuhamasishe utumiaji wa nishati mbadala au jadilifu (renewable energy). Kodi ipunguzwe katika uagizaji wa vifaa hivyo nje ya sola ambayo haina kodi kwa sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri gharama za ukaguzi na leseni kibali cha NEMC ipunguzwe ili Watanzania wengi zaidi waweze kutafuta hivyo vibali badala ya kusubiri kupigwa faini ambayo wanaona ni ndogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vyanzo nashauri asilimia kumi ya tozo zote au leseni zinazotolewa na zinahusiana na masuala ya Mazingira. Mfano; leseni ya Viwanda vyote, leseni za Madini, Leseni za Ujenzi, Leseni za Utalii, Leseni za huduma za Afya Mawasiliano, Uvuvi, Mifugo, Kilimo na Leseni za uzalishaji wa Nishati. Pia tozo tunayopata kutokana na (TFS - Wakala wa Misitu Tanzania) ambayo ni uvunaji wa misitu yetu asilimia ishirini ya mapato hayo yarudi kuboresha mazingira. Leseni au vibali vya watumiaji maji asilimia kumi pia zirudi kuboresha vyanzo vya maji katika Mfuko wa Mazingira pia tuliweka kodi ya kuingiza magari na bidhaa chakavu huwa zinaharibu mazingira, asilimia ishirini ya mapato hayo yaende katika Mfuko huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza shilingi kumi ya kila lita ya mafuta pia iende kwenye Mfuko wa Mazingira. Pia shughuli zote zinazofanyika ambazo zinaharibu mazingira, pawe na asilimia kumi ya tozo kwenye vyanzo hivyo vinavyopatikana ili mfuko uweze kuwa endelevu na mipango itimizwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Fedha za EWURA, pia asilimia kumi ziende kwenye kuboresha au kutunisha mfuko. SUMATRA pia katika leseni zote ichangie asilimia kumi ya mapato yake katika mfuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuleta hamasa incentive pawe na ruhusa kuweka angalau asilimia tatu au tano kama gharama expenses ambayo itatozwa kodi (allowed expense) katika balance sheets (Income Tax Act) na itafanya makampuni yachangie katika masuala ya mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanaoshughulika na utalii wapewe maeneo maalum ya kuboresha mazingira na hivyo hivyo viwanda, migodi na biashara zote zipewe maeneo maalum ya kusimamia na kuboresha mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi iondolewe katika mitambo ya kusafirisha na kurudisha bidhaa sokoni recycling na pia katika mitambo ya kufua umeme unaotokana na taka ngumu. Tuwe na tozo ya shilingi hamsini kwa kila mfuko wa mbolea ya dukani inayoagizwa kutoka nje ya nchi. Tunaweza kujadili na pakawa na Tume Maalum ya kuangalia vyanzo vya Mfuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.