Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote mwananchi wa Temeke hasa wakazi wa chang’ombe na Keko wanamshukuru Mheshimiwa Mpina kwa ziara zake zilizotokana na kero ya muda mrefu katika eneo lao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na yote hayo bado nguvu kubwa ya kukomesha wachafuzi wa mazingira inahitajika. Bado baadhi ya viwanda vinatiririsha maji machafu kwenda mitaani na baharini. Tafadhali Mheshimiwa Mpina usichoke kuja Temeke ili tuzitatue kero hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho napenda Mheshimiwa Waziri ashauriane na Waziri wa TAMISEMI ili watoe maelekezo kwa Halmashauri kuwa Kamati ya kutoa vibali vya ujenzi imjumlishe na Afisa Mazingira wa Halmashauri badala ya Mganga Mkuu. Hii itasaidia kuhakikisha hakuna kibali cha ujenzi kitakachotolewa bila tathmini ya mazingira. Kwa sasa hali hii ni mbaya na vibali hutolewa hata katika maeneo oevu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.