Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri wanazozifanya. Mazingira ni jambo muhimu sana katika maisha ya binadamu. Naiomba Serikali itilie mkazo sana katika suala zima la uhifadhi wa mazingira pamoja na juhudi za Serikali katika kuongeza kasi ya upandaji wa miti, lakini bado kuna mambo mengi sana yanayosababisha uharibifu wa mazingira nayo yafanyiwe kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali wakae pamoja na taasisi nyingine katika kuweka sawa sheria ya mazingira kwa kuwa wananchi wengi wanapotafuta vibali mbalimbali vya ujenzi kunakuwa na vikwazo vingi sana. Mambo yanayowekwa kwa Mtanzania wa kawaida inakuwa vigumu kuyatekeleza kwa haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze Serikali kwa kufuatilia kwa kina kuangalia viwanda ambavyo vinakiuka taratibu za mazingira. Hiyo imesaidia sana Temeke kutokana na matatizo ya Serengeti Breweries.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.