Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara iweke utaratibu wa kushirikiana na halmashauri kwa ajili ya miradi ya utunzaji wa vyanzo vya maji kwa kuweka miradi ya kilimo au vinginevyo kwa ajili ya vijana kwenye umbali unaokaribia mita 60 za hifadhi za kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wilaya kadhaa ikiwemo Biharamulo zina maeneo makubwa ambayo ni hifadhi za Taifa. Mfano 54% ya eneo la Wilaya ya Biharamulo ni hifadhi za Taifa, kwa sababu hiyo wananchi wanalazimika kutunza hifadhi na mazingira kwa kuwa population density ni kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna haja ya Wizara hii kubaini wilaya zote za aina hii na kukaa nazo na kubuni suluhisho la pamoja kwa maana ya kupata rasilimali fedha pamoja na utashi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeongelea vijana kupewa miradi kwenye maeneo karibu na mita 60 za hifadhi ya vyanzo vya maji, lengo ni kuwatumia vijana, wawe walinzi wa vyanzo vya maji wakati wakitekeleza miradi yao katika maeneo jirani na vyanzo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna ushahidi kuwa asilimia kubwa ya mkaa unaotengenezwa hapa nchini unatumika katika Jiji la Dar es Salaam na Majiji mengine. Je, Serikali haioni haja ya kuweka tozo kwenye kila gunia la mkaa unaoingia Jiji la Dar es Salaam kutumia tozo hiyo kutoa ruzuku kwa matumizi ya gesi ili wananchi wanunue mitungi ya gesi kwa bei ya chini.