Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. WAITARA M. MWIKWABE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa maoni yangu katika suala la mazingira. Ni muhimu Wizara ya Mazingira na Muungano ibainishe na kutambua maeneo ambayo watu wamejenga katika kingo za mito na mabonde.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba maeneo hayo yatambuliwe na kuagiza wahusika wote wahame kwa mujibu wa Sheria na hili lisimamiwe wakati wote sio wakati wa mvua tu na kila mtu ajue kwamba maeneo hayo hayajengwi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri sheria itekelezwe wakati wowote na Viongozi wa Serikali ambao watahusika kuuza au kushawishi watu kujenga au kuwaandikia vibali ili waishi kwenye kingo na mabondeni washughulikiwe kisheria ili kuondoa malalamiko na usumbufu wakati wa mvua.