Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi ya mazingira kampeni ya utunzaji wa mazingira; iwepo kampeni ya utunzaji wa mazingira kwa wananchi wote kuanzia mashuleni, Vyuoni, Vitongoji, Kata, Vijiji, Wilaya, Mikoa na Taifa. Mkakati uwekwe wazi ili kila mwananchi ajue faida za utunzaji wa mazingira na hasara za kinyume chake mfano mito kukauka, ukosefu wa mvua na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kampeni ya upandaji miti; iwekwe au iandaliwe kampeni ya upandaji miti kwa kila kaya na kuhakikisha inakua kampeni/zoezi endelevu, mfano kila kaya ipande miti 10 kila mwaka na kuhakikisha inakua. Halmashauri zihakikishe zinaandaa vitalu vya miche kila mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kampeni ya kuzuia ukataji wa miti na uchomaji moto; kampeni hii iwe ni ya kuhakikisha miti inalindwa na wananchi wenyewe, kampeni kama “Panda Miti Kata Mti”, wavunaji halali wa miti. Halmashauri zote ziwe na Sheria ndogo za kudhibiti uchomaji moto wa misitu/mapori, hii italinda misitu yetu na miti hivyo kuokoa vyanzo vya maji. Wenzetu Burundi ni kosa kubwa kuchoma moto au kukata miti.
Mheshimiwa Mwenyekiti,Serikali ishughulikie nishati mbadala ya mkaa ili kupunguza matumizi ya mkaa na hiyo kuokoa miti na misitu kuteketea mfano, Watanzania wanufaike na gesi ya Mtwara kutumika majumbani kwa gharama nafuu Affordable cost, haiingii akilini mtungi wa gesi kuuzwa kwa Shilingi 55,000- 60,000 kule Kakonko (Kigoma), wakati gesi ipo nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, athari ya wakimbizi kwenye mazingira, Mkoa wa Kigoma una wakimbizi wapatao laki tano kwa sasa toka Burundi na DRC wakimbizi hawa wanatumia kuni kupikia hivyo wanakata miti kila siku. Hivyo miti 500,000 inatumika kama kuni kwa siku kwa mwaka ni miti 182,500,000 kiasi ambacho hakina replacement yake kwani haipandwi miti mingine. Mapendekezo; UNHCR wahakikishe wakimbizi wanapikia gesi ili kuokoa uharibifu wa miti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, viroba vilivyokamatwa vilitozwa kodi na ilikuwa biashara halali, hivyo wamiliki waruhusiwe kuuza ili kulinda mitaji yao. Serikali ingezuia uzalishaji ikatoa muda wa kuvimaliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kero za Muungano zielezwe wazi kwa wananchi wote na wananchi waelezwe kama kweli wanaridhika na jinsi Muungano unavyokwenda. Ni muda muafaka sasa wananchi waulizwe kama wanataka Muungano au la ili isionekane Serikali inawaburuza wananchi au kuwa lazimisha kuwa kwenye Muungano. Magari yaliyosajiliwa ZNZ kwa nini yakiwa bara yanatozwa ushuru tena kwa vile yanatoka nchi nyingine wakati ni nchi moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, CCM Zanzibar ikae na CUF ili kuleta muafaka juu ya maridhiano. Haileti afya ya kitaifa kuendelea kuishi kibabe hasa CCM wanapojinadi kuwa hawako tayari kukaa na CUF kutafuta muafaka au suluhu, duniani kote wagombanao ndio wapatanao.