Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

Hon. Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira

MHE. MARTHA J.UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa mchango wangu kwa hoja hii kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuthamini shughuli ndogo ndogo za wananchi katika kuzalisha mali, lakini naomba kutoa masikitiko yangu kuhusu wajasiriamali wadogo wanaonyweshea mbogamboga kutumia maji machafu yanayotiririka kwenye mifereji, Jijini Dar es Salaam. Mboga hizi huuzwa kwenye mahoteli mbalimbali jijini humo na kusababisha madhara kiafya pia inasababisha kinyaa kwa walaji. Kero hii inajulikana na watu wengi wakiwepo viongozi wanaoweza kufanya uamuzi kupiga marufuku kutumia maji hayo. Vinginevyo Serikali ishughulikie kusafisha mifereji yote michafu ili maji yanayotiririka humo yawe salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na Sekta ya Kilimo, kuna athari kubwa sana ya uharibifu wa mazingira kwa mfano robo tatu ya ardhi ya Wilaya ya Kiteto imelimwa, (kuacha mapori yasiyofaa kwa kilimo na ufugaji) kwa sababu hiyo miti yote katika maeneo hayo yamekatwa na ardhi kubakia tupu (bila miti). Nini mikakati ya Serikali katika kunusuru Wilaya hiyo (ardhi yake) kugeuka kuwa jangwa? Tuliambiwa ardhi hiyo imepimwa miaka mitatu iliyopita, lakini hadi leo wakulima wakubwa wanaendelea kulima na ardhi inaendelea kuwa finyu pia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bajeti ya Sekta hii; sehemu kubwa asilimia 80 inategemea fedha za nje, hali inayohatarisha kutekelezeka kwa miradi ya mazingira kwa sababu fedha za nje mara kwa mara haziletwi kwa wakati. Naomba kujua Serikali inasemaje kuhusu hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.