Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na shukrani kwa kuingiza katika mpango
(a) Ukarabati wa meli ya MV. Butiama; na
(b) Ujenzi wa barabara ya Bunda-Kisovya-Nansio.
Mheshimiwa Naibu Spika, Naomba yafuatayo yawekwe katika Mpango:-
Kwanza, Ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi katika Kisiwa cha Ukerewe; jambo litakalowasaidia vijana kupata msingi wa kujiajiri na kupunguza utegemezi wao katika Ziwa Victoria kwenye shughuli za uvuvi na kwa sababu hawana uwezeshwaji, wanajiingiza katika uvuvi haramu.
Pili, ujenzi wa Daraja la kuunganisha Kisorya (Jimbo la Mwibara) na Lugezi (Wilaya ya Ukerewe) ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha mawasiliano ya kijamii na kiuchumi na hivyo kuimarisha hali ya maisha ya wananchi wa Kisiwa cha Ukerewe. Hivyo Daraja hilo nashauri liwekwe katika Mpango.
Tatu, utafiti wa udongo katika Kisiwa cha Ukerewe na maeneo mengine ambayo udongo umechoka, itasaidia kupunguza upungufu wa chakula kwani utafiti utasaidia kujua aina ya mazao tutakayopaswa kulima kulingana na aina ya udongo kulingana na utafiti.