Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nashukuru kupata fursa hii lakini kabla sijasema naomba niweke sawia mambo mawili yaliyojitokeza jana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mtu jana alijaribu kuonesha kwamba Mwenyekiti wa Kambi Rasmi ya Upinzani ni mtu wa kawaida, lakini naomba niweke rekodi vizuri, Mheshimiwa Freeman Mbowe, alikipokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo kikiwa na Wabunge watano, lakini amekipeleka na akafika mahali mpaka ikaundwa UKAWA na leo Bunge hili lina Wabunge kutoka upinzani zaidi ya 100. Lakini ameweza kuunganisha nguvu na hata akatuletea magwiji wa siasa kutoka huko kwenu ambao wakikaa kimya CCM wote mnakusanyika kufukiria kwa nini yupo kimya. Kwa maana hiyo Mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe ni profesa wa sayansi ya siasa, niweke rekodi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile jana kuna baba yangu alisema kwamba mama yetu Ruth Mollel kwamba eti kwa sababu amewahi kuwa kiongozi mkubwa katika nchi hii hastahili kuwa kwenye chama cha upinzani kwa sababu ana siri za Serikali. Ninataka niwaambie kwamba CCM sio masijala ya siri ya Tanzania. CCM ni chama kama chama kingine cha siasa, CCM ni kana CHADEMA ni kama CUF na mtu yeyote haijalishi ameshika nafasi katika nchi hii anaruhusiwa kuwa kwenye chama chochote ilimradi havunji Katiba ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefanya utafiti kuanzia miaka ya 1970 mpaka 2016 nimegundua ili kutekeleza mpango kazi wa mwaka mmoja katika nchi hii unahitaji miaka mitatu mpaka minne kwa hiyo sitazungumzia pesa kwa sababu nchi hii haina pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitakwenda kujikita tubadilishe fikra kwa babu fikra ndiyo tatizo leo kwa hiyo tukibadilisha namna tunavyofikiri nchi hii itakuwa na pesa na tunaweza kukabiliana na matatizo yaliyotukabili mbele. Wakati nawaza hilo, nikafikiria, hivi katika kubadilisha fikra na kuisadia nchi hii, solution ni kubana demokrasia? Ni kuzuia uhuru wa kutoa mawazo ya Bunge? Ni kuhakikisha vyombo vya habari havifanyi kazi yake vizuri? Nikagundua la hasha, kuruhusu uhuru wa mawazo ndipo tutakapogundua magwiji wa fikra katika nchi hii.


Mheshimiwa Mwenyekiti, sifa ya magwiji wa fikra ni watu wenye uwezo wa kufikiri katika upeo ulipitiliza ubongo na sifa yake ni kwamba huko hakuna unafiki, hakuna uzandiki, hakuna u-CCM wala u-CHADEMA, tunalifikiria Taifa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme, Rais wa Marekani alipokuwa anamkabidhi Makamu wake kazi, alimwambia naamini akili zako sana, akamwambia ninakupa mission ya kupeleka nchi yetu iwe nchi ya kwanza kufanya miujiza katika sayari ya mars. Tujiulize sisi tunapokabidhiana madaraka, tunakabidhiana madaraka kwa ajili ya kuishughulikia upinzani, kwa ajili ya kubonyeza demokrasia, tunakabidhiana madaraka kwa ajili ya kufanya nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tujiulize kwa nini Marekani wanataka kwenda mars, wanataka wawepo, pamoja na mambo mengine, wawe wanaitazama dunia wakiwa mbali wanaiangalia Tanzania, wanaangalia mabara yote na mtu yeyote akitaka kuigusa Marekani wakati akiwa katikati ya Bahari ya Atlantiki, anagongwa kabla hajaifikia Marekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tujiulize sisi kama nchi, hivi tunajisifia kwa kutegua mtego wa Mheshimiwa Nape kuongea na waandishi wa habari halafu tunasema tumetumia akili na Usalama wa Taifa una akili sana katika nchi hii! Nchi yetu leo tunauliza maswali ya msingi kwamba Ben Saanane yuko wapi? Hatuna hata uwezo wa kueleza yuko wapi na ninategemea kwamba Usalama wa Taifa ndiyo darubini ya nchi, ndiyo maana tunaita TISS, ile ‘I’ ndicho kitu cha msingi; intelligence! Uwezo wa kutazama na kuona mambo yasiyoonekana kwa macho ya kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nchi inahangaika, Mwenyekiti wa Kambi ya Upinzani anasema, tuombe basi msaada Uingereza kwa watu wenye darubini ya kutazama mambo yasiyoweza kuonekana, tunazunguka zunguka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme hivi, hii nchi siyo ya CCM, siyo ya CHADEMA, ni yetu wote Watanzania. Ni lazima tuanze kufikiri ni namna gani tunaweza kuisaidia Tanzania na tunatokaje sehemu hiyo ambayo sasa tupo. Juzi hapa na jana limejadiliwa suala la East Africa. Tumeingia kwenye uchaguzi na ningependa sana Spika angekuwepo hapa. Unajua ukiwa umelala uko nusu usingizi, huwa kuna akili nzuri zinakuja, lakini hizo akili huwa zinakuja wakati kuna msiba umetokea mkubwa wa mtu ambaye mnampenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipokuwa hapa kwenye msiba wa Sitta, Mheshimiwa Spika ndipo alipofikia akagundua sisi tunapita tu hapa duniani, akasema anatamani sana kufikia hata nusu ya utekelezaji wa Mheshimiwa Sitta, lakini juzi tumefanya uchaguzi wa East Africa hapa, yamefanyika madudu. Nataka umwambie Mheshimiwa Spika, huu mtego wa uchaguzi wa Afrika Mashariki ni mtego ambao unamfanya hata aweke milestone ya kwanza kumwelekea Sitta, hata kufikia nusu ya Mheshimiwa Sitta. Ndiyo mtego wa kwanza ambao tunampa Bunge hili. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vita kuhusu East Africa na uchaguzi wa East Africa siyo kati ya CCM na CHADEMA, ni kati ya Tanzania na dunia ya kibiashara na vita vya kibiashara vya kidunia. Tunahitaji akili kubwa kama ya Mheshimiwa Masha ambaye amewahi kuwa kiongozi ndani ya Serikali, anajua Usalama wa Taifa vizuri namna ya kushirikiana nao, anajua nchi hii ili tuweze kuunganisha nguvu tupambane kwenye vita vya kidunia katika uchumi wa dunia, siyo kutafutana na kutafuta CHADEMA nani mzuri nani mbaya. Hicho ndicho tunachokifikiria; tuache kuwaza katika akili ndogo. Bahati nzuri, tunaye Mheshimiwa Waziri mzuri, msikivu na mwelewa tumtumie, ni fursa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu yangu Waziri wa TAMISEMI nikwambie tu, unaye Naibu wako mzuri ambaye ametuonesha mfano mzuri wa utawala bora, Mheshimiwa Jafo.

Mheshimiwa Jafo amekuja kwenye Wilaya ya Siha, ametuunganisha wana-CHADEMA na wana-CCM tukaanza kuwaza tu kuhusu maendeleo ya Wilaya yetu, akaacha mambo ya uchama ili twende mbele. Tunataka viongozi kama hao, hatutaki watu ambao wanakuja kwa shughuli za Kiserikali wanaanza kufikiria mambo ya vyama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu, usalama wa nchi ni uchumi. Tujiuize maswali ya msingi, Usalama wa Taifa kama ina microscopic eyes na tunazungumzia hapa na wakati mwingine tukizungumzia Usalama wa Taifa watu wanafikiri tunadhalilisha Usalama wa Taifa, hapana tunatafutia Usalama wa Taifa uhuru wake na waanze kupelekwa Usalama wa Taifa watu wenye akili kubwa, ndicho tunachokipigania hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tujiulize Kagoda ilivyokuwa imetokea, Richmond, EPA; Usalama wa Taifa walikuwa wapi? Leo Rais anahangaika na makontena huko, tujiulize kama hilo wazo la kuruhusu makontena yaende nje lilikuwa baya, Usalama wa Taifa walikuwa wapi wasimshauri Mheshimiwa Rais? Tujiulize kama Mheshimiwa Rais leo atakuwa amekosea kuzuia hayo makontena, Usalama wa Taifa wako wapi kama Mheshimiwa Rais wetu atakwenda kukosea kwa maana ya uamuzi huo anaofanya? Hiyo ndiyo akili tunataka nchi yetu isaidiwe na iongozwe kwa namna hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu zangu tujiulize hivi hawa watu wanaompelekea Mheshimiwa Rais message kwamba kuna muuza duka huko amemtukana halafu muuza duka anakwenda kusimama na Rais Mahakamani eti ana kesi na Mheshimiwa Rais, ni nani huyo anayempelekea Mheshimiwa Rais anaanza kufuatilia mambo madogo madogo katika nchi kama hii maskini ambayo asilimia 48 ya bajeti yake inategemea misaada kutoka nje? Kuna mambo makubwa ya kumwelekeza Mheshimiwa Rais ili ayafikirie, siyo kuwa na kesi na watu wadogo wadogo wa mtaani kwenye shughuli za simu. Tuanze kutafakari, tuanze kufikiria, tuipeleke nchi yetu inavyotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua nawatibu akili, mimi ni Daktari wa binadamu, tuanze kuwaza, Mheshimiwa Mwinyi unanielewa. Ukianza kuona mtu ana Ph.D halafu anajipendekeza kwa mkubwa kwa sababu tu huyo mkubwa anafanya mambo ya uteuzi, ni mojawapo ya kujitambua na kupima kwamba uwezo wako wa kufikiri ni mdogo, hata kama ulifaulu, ulikuwa na IQ ndogo tu ambazo zingekuwezesha kufaulu matokeo darasani, lakini IQ ni ndogo sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu tuanze kujipima IQ, zetu ni kwa nini mtu mwenye Ph.D anajipendekeza kwa mtu mkubwa? Inakuwaje zero inapigiwa salute na majeshi yetu? Mheshimiwa Mama Ndalichako anza kujiuliza, hivi kuna leakage gani inapitisha zero mpaka inakuwa Mkuu wa Mkoa katika nchi hii? Inatokeaje? Hatuwezi kukubali hicho kitu. Hizo zero hatuzidharau, tujiulize, hivi kama yeye ameweza ku-shake nchi mpaka Ph.D inampigia salute, tujiulize sisi wenye Ph.D na huyo mwenye zero ni nani mwenye akili zaidi? Hilo ndiyo la msingi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tujiulize, mimi nawarudisha, siwezi kuzungumzia tena maji maana naona…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Muda wako umekwisha!