Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza kabla ya kuendelea nianze na quotation moja aliitoa mtaalam mmoja wa masuala ya uongozi anaitwa John Maxwell, anasema hivi:- “If you want to recognize the intelligence of the leader look people around him.”
Mheshimiwa Naibu Spika, kama Mkuu wetu wa Nchi amezungukwa na watu aina ya Goodluck amezungukwa na watu aina ya Bashite what do we expect. (Kicheko/ Mheshimiwa Naibu Spika, sikutegemea kama tunaweza kuwa na aina ya viongozi ambao wanaweza kuja Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kuchangia katika suala zima la utawala bora baadaye nitamalizia na utumishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu kwa sasa hivi imekumbwa na tatizo kubwa sana katika suala la uchumi na tatizo hili linatokana na ukosefu wa utawala bora katika Taifa letu. Leo hii nchi yetu tumekosa fedha za MCC takriban Dola 463,000,000 kutoka Marekani kwa sababu ya ukosefu wa utawala bora. Leo hii tumekosa mikopo kutoka nje.
Mheshimiwa shemeji yangu naona hayupo hapa leo, Mheshimiwa Waziri wa Fedha, amekwenda Ulaya, amezunguka nchi zote, amekosa mikopo kwa sababu kigezo namba moja cha mkopo ni lazima kuwe na good governance katika Taifa, lakini tunakosa fursa hizi kwa
kutokuwepo na utawala bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka leo Bajeti ya Mwaka 2016/2017, imetekelezeka kwa asilimia 34 tu kwa sababu kubwa ya ukosefu wa utawala bora. Wakati huo huo tunakosa misaada kutokana na ukosefu wa utawala bora katika Taifa hili. Wawekezaji wanakimbia, wafanyabiashara wanakimbia; kwa sababu hakuna mwekezaji ambaye ana akili timamu anaweza kuwekeza kwenye nchi ambayo muda wowote mkataba unaweza ukavunjwa kwenye majukwaa. Hakuna mwekezaji ambaye anaweza kuwekeza kwenye nchi ambayo haifuati misingi ya utawala wa Sheria , hakuna.
Mheshimiwa Naibu Spika yapo mambo humu ndani tunaweza kutofautiana kwa sababu ya itikadi zetu, lakini yapo mambo ambayo lazima tuungane kwa ajili ya maslahi ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, utawala wa sasa unaendeshwa kwa double standard, Serikali haina consistency. Kwa mfano unaweza kukuta kwamba watu ambao wako ngazi ya chini wanavunja Sheria na wanachukuliwa hatua kali, lakini wapo watu ambao wapo kwenye mamlaka kubwa wanavunja sheria na wakati mwingine wanalindwa mpaka na mitutu.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi binafsi ni mdau mkubwa sana wa vita juu ya ufisadi, lakini jitihada za Mheshimiwa Rais wetu zinakosa uhalali kwa sababu ya kuwa na double standard. Kuna maeneo anaonekana anachukua hatua na kuna maeneo anaonekana hachukui hatua.
Mheshimiwa Naibu Spika, mkutano uliopita kuna suala nililizungumza humu ndani, nilizungumzia suala la uvunjaji wa Sheria ya Finance Act ambayo iliundwa mwaka 2012 section namba 29 inasema kwamba hakuna transfer share yoyote ambayo itafanyika bila kulipwa Capital Gain Tax.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kampuni inaitwa Shell ilifanya transfer share kutoka kampuni ya BG. Shell ilinunua vitalu vya gesi kutoka kampuni ya BG, lakini hakuna Capital Gain Tax ambayo imelipwa. Cha kusikitisha sana wakati tupo kwenye Kamati, Mkutano uliopita niliuliza viongozi wa FCC wakasema kwamba swali lako tutajibu kwa maandishi mpaka leo hawajajibu. Nika-take trouble kupitia Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge, section namba 29 nikasema kwamba, toeni sababu kwa nini mpaka leo Capital gain tax haijalipwa lakini mpaka leo, toka tarehe nne TRA nao hawajajibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Muhongo alijaribu kupiga bla bla, lakini nashukuru alikiri kwamba kuna wizi unafanyika kwenye makampuni haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii kampuni ya Shell, hii ni kampuni ambayo wiki mbili zilizopita, nina ushahidi hapa, imekuwa reported kwenye vyombo vyote duniani kwamba imetoa rushwa ya trilioni mbili kwa ajili ya kukidhi maslahi yake kwenye Serikali ya Nigeria. Baada ya kugundulika ndipo wakaamua kuitumbua.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa sisi kwenye Serikali yetu kampuni hii lazima tuone kwamba kuna harufu ya rushwa hapa. Haiwezekani fedha za wananchi takribani dola milioni 500, takribani kama trilioni moja na ushee, ni hela nyingi sana, zinaweza kutengeneza hiyo standard gauge ambayo Mheshimiwa Rais anataka kuitengeneza kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro; lakini imepotea katika mazingira hayo na hakuna ambaye amechukuliwa hatua na vitu vinafunikwa funikwa na hakuna ambaye anahoji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama kweli Mheshimiwa Rais wetu anataka tutengeneza imani na yeye, aanze kuchukua hatua ambazo zinalenga kote kote, achukue hatua kwa watu wake, achukue hatua kwa watu ambao anafikiri kwamba hawamuhusu, wote kwa pande zote mbili
achukue hatua kwa sababu mnatupotezea imani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa haraka haraka naomba pia nichangie upande wa utumishi. Kuna uhusiano mkubwa sana kwenye suala la uwajibikaji na maslahi, hivi vitu viwili vinakwenda sambamba. Hapa nilipo nina chati kutoka Chuo cha Walimu, Kanda ya kati lakini nitaongelea
specifically Singida. Walimu wa Mkoa wa Singida toka mwaka 2013 mpaka leo hawajapa stahiki zao, takribani bilioni 2.4.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatuwezi kutegemea matokeo makubwa Singida na ndiyo maana elimu imekuwa ikianguka kila siku, tumegundua miongoni mwa sababu ni pamoja na hii. Naomba niishauri Serikali jambo moja; kama ambavyo wanafanya kwa wakandarasi, mkandarasi anapokuja kulipwa fidia zake, anapokuja kulipwa malipo yake analipwa kwa riba. Vivyo hivyo tupeleke utaratibu huu kwa upande wa watumishi wa Serikali, specifically Walimu pale mnapokuja kuwalipa muwalipe kwa riba kwa sababu fedha zile kwa wakati ule value yake ni tofauti na wakati huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Mheshimiwa Waziri atutazame upya kwa sababu inasikitisha sana elimu yetu imekuwa ikisuasua kwa muda mrefu sana na Walimu wamekuwa wakilalamika sana, wanaishi maisha magumu, wanakosa stahiki zao. Moja kwa moja hiyo automatically inapelekea utendaji mbovu kwenye elimu wanayoitoa kwa wanafunzi wetu. Tutaendelea kuzalisha watoto ambao hawana vigezo, hawana sifa, kwa sababu tunashindwa kuwasaidia Walimu kupata stahiki zao.