Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia fursa hii ili nami nipate kuchangia Hotuba za Bajeti mbili hizi, Wizara ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Utumishi na Utawala Bora Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetujalia uzima na afya njema. Nielekeze pongezi zangu kwa Mheshimiwa Waziri, George Simbachawene pamoja na dada yangu, Mheshimwa Waziri, Angella Kairuki kwa hotuba nzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, teknolojia inakuwa kwa kasi sana siku hizi. Leo tumeshuhudia maelezo hapa mtu anamaliza semester mbili ndani ya miezi minne, habari kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi leo nimefunga, nimefunga kwa maana nina swaumu au nimejizuia kula. Nimefanya hivyo kwa makusudi tu ili nimwombe Mwenyezi Mungu aniongoze katika haya nitakayoyazungumza leo niseme iliyo kweli, basi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye kitabu ambacho nakiamini cha Quran, Sura ya 33, Aya ya 70 baada ya audhubillah mina shaitwan rajim, Mwenyezi Mungu anasema Bismillah Rahman Rahim; ya ayuha ladhiina aamanuh, takkullah wakulu kaulan sadida. Hii ni Aya ya Mwenyezi
Mungu. Tafsiri yake; Enyi mlioamini mcheni Mwenyezi Mungu, muabuduni Mwenyezi Mungu na semeni kauli zilizo za kweli’”
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mwenyezi Mungu aniongeze niseme ile iliyo ya kweli. Wilaya ya Mafia, Hospitali ya Wilaya ya Mafia ambayo mimi ni Mbunge wao haina huduma ya X-ray takribani miaka minne sasa. Nilipokuwa najinadi niliwaahidi wananchi wa Mafia kwamba
nikipata fursa hii nitajitahidi kushirikiana na watu mbalimbali Hospitali ya Mafia iwe na X-ray mpya kabisa. Nimetimiza, true to my words, nimetimiza ahadi hiyo, mwezi wa Nne mwaka wa jana.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa masikitiko makubwa sana huu ni mwezi wa Nne mwaka 2017. Mwezi wa Nne mwaka 2016, X-ray machine ile mpya imefika Mafia na katika nukta hii kwa namna ya kipekee kabisa ningeomba nitambue msaada mkubwa sana aliyeutoa mama yetu kipenzi, Mheshimiwa Salma Kikwete alipokuja Mafia. Sina uhakika kama kanuni zinaruhusu Mbunge anayeongea ampigie makofi Mbunge aliyekaa, lakini naomba Bunge tumpe makofi makubwa sana Mheshimiwa mama Salma.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya X-ray ile kufika Mafia zikaanza figisufigisu. Mtu wa kwanza; na bahati mbaya simwoni hapa; Mheshimiwa Waziri wa Afya; akatuambia kwamba hamruhusiwi kuifunga kwa sababu tuna mkataba na Kampuni inaitwa Philips na kampuni hii ndiyo pekee
inayoruhusiwa kufanya ukarabati na matengenezo ya ile Xray ya zamani. X-ray ya zamani ni chakavu, ni ya teknolojia ya miaka ya 1970, ukiitengeneza inaharibika. Sasa leo wanasema kuna mkataba na Philips, mpaka leo umefika sasa mwaka mmoja X-ray ile bado ipo kwenye stoo, nawauliza wahusika wanatuambia mkataba.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mafia ni kisiwa, huna namna kusema kwamba labda mgonjwa utamhamishia hospitali ya jirani, sasa wagonjwa wetu sisi referral hospital yetu lazima umpandishe kwenye boti kwa masaa tano kwenda, referral hospital Temeke.
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi nilikuwa huko wakati wa Pasaka, tumepeleka wagonjwa wawili Hospitali ya Temeke, tunafika Temeke na kwenyewe nako tunaambiwa X-ray ni mbovu kwa zaidi ya mwezi mmoja, haohao Philips. Tunawauliza wahusika wanasema mkataba na Philips umekwisha toka mwaka wa jana. Mafia tunazuiwa tusifunge kwa sababu kuna mkataba na Philips, Temeke wanasema X-ray mbovu Philips mkataba umekwisha, tushike lipi? Hili la Temeke watalizungumza wenyewe akina Mheshimiwa Mangungu na Mheshimiwa Mariam Kisangi na ndugu yangu
Mheshimiwa Mtolea lakini mimi najikita kwenye Mafia.
Mheshimiwa Naibu Spika…
T A A R I F A...
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba naipokea Taarifa ya Mheshimiwa Waziri kwa tahadhari kubwa sana. Kwanza hajanipa time frame, kwa sababu hili jambo limekuwa likienda kwa danadana kwa muda mrefu sana. Hicho chumba ambacho wamekitoa mwanzo walisema sisi wenyewe tujenge halafu tuhamishie ile mashine mpya kule. Midhali yeye amesema leo kwamba
wametupatia chumba hicho; mimi nafahamu kule hatuna chumba cha ziada; lakini kama ataweza kutupatia kingine cha kujenga haraka kwa hizo milioni 50, tutashukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, labda niliache hili suala kwa sababu nilikuwa nilielezee kwa upana zaidi. Niingie kwenye suala la pili. Kwenye ukurasa wa 11 wa Hotuba ya Mheshimiwa Waziri amezungumzia migogoro ya mipaka baina ya wilaya, mikoa, vijiji na vitu kama hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kule Mafia mipaka yetu ni bahari, hakuna namna nyingine ya kupakana na kijiji cha karibu, tunaopakana nao karibu ni ndugu yangu Bwege kule upande wa Kilwa. Tungeomba sana mipaka ya bahari ije iwekwe, kwa sababu kule mafia kuna exploration za mafuta zinafanyika, kwa kiasi kikubwa sana zimo ndani ya eneo la Mafia lakini kutokana na logistics yale makampuni yanafanya
wakitokea Kilwa. Sasa matokeo yake chochote kinachopatikana kinaonekana ni sehemu ya Kilwa wakati kimipaka, kihalisia ile ni sehemu ya Mafia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunaomba sana wataalam watakapokuja, sijui wanatumia vitu gani vya kisayansi ili kutofautisha mipaka kwenye bahari lakini waje watuoneshe. Kuna kisiwa kimoja kinaitwa Kisiwa cha Ukuza, kisiwa hiki ni sehemu ya Mafia, lakini shughuli zote za kijamii zinafanyika kutokea Kilwa, tungeomba sana Mheshimiwa Waziri hilo nalo atusaidie kutupatia ufafanuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, zahanati; tumeomba zahanati…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Dau, naambiwa muda wako umekwisha.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.