Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. George Mcheche Masaju

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipatia fursa hii na mimi niweze kuchangia. Nikushukuru wewe mwenyewe Mheshimiwa Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wote wa Bunge kwa namna ambavyo mnasimamia
uendeshaji wa shughuli za Bunge hili kwa ufanisi mkubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii baada ya kuwa nimesikiliza mjadala huu na mimi nichangie kwa kushauri mambo ambayo yamejitokeza, mambo ya kikatiba na kisheria. Bunge ni taasisi muhimu sana kwa mustakabali wa Taifa lolote lile, ndiyo maana wanapewa jukumu la kutunga sheria. Kwa sababu ya umuhimu huo mimi nitambue umuhimu wenu ninyi Waheshimiwa Wabunge ni watu muhimu, your so much very important person, ndiyo maana mnaitwa Waheshimiwa, lakini Bunge hili nalo lina utaratibu wake wa kufanya kazi; na majukumu ya Bunge yametajwa katika Katiba Ibara ya 63 inaeleza vizuri majukumu ya Bunge.
Mheshimiwa Spika, Ibara ya 63(2) inasema; “ Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka kwa niaba ya wananchi, kusimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii.
(3) Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge laweza-
(a) kumuuliza Waziri yeyote swali lolote kuhusu mambo ya umma katika Jamhuri ya Muungano ambayo yapo katika wajibu wake;
(b) kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa bajeti;
(c) kujadili na kuidhinisha mpango wowote wa muda
mrefu au muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya Muungano na kutunga sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango huo; (d) kutunga sheria pale ambapo utekelezaji unahitaji kuwapo sheria; na
(e) kujadili na kuridhia mikataba yoyote inayohusu Jamhuri ya Muungano ambayo kwa masharti yake inahitaji kuridhiwa.
Mheshimiwa Spika, pia Bunge limepewa uhuru wa mijadala humu ndani, Ibara ya 100. Lakini Ibara ya 100(2) imeweka masharti kuna mipaka, Ibara ya 100(2) ya Katiba inasema hivi; “Bila kuathiri Katiba hii, au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, Mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa sharti la madai mahakamani kutokana na jambo na lolote alilolisema au kulifanya ndani ya Bunge, au alileta Bunge kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.” Katiba hii pia imegawa madaraka katika mihimili mitatu ya dola ambayo ni Bunge lenyewe, Mahakama na Utendaji.
Mheshimiwa Spika, Bunge linatunga sheria na kuismamia Serikali utekelezaji wake, Mahakama inatafsiri sheria inatoa haki na Serikali kwa maana ya utendaji, inasimamia utekelezaji wa sheria zilizotungwa na Bunge.
Katiba hii inaposema kwamba bila kuathiri masharti haya ina maana kwamba Bunge lazima ifanye kazi zake kwa mujibu wa sheria. Ndiyo maana sasa Ibara ya 26 ya Katiba inaeleza kila mtu ana wajibu wa kuifuata na kuitii Katiba hii na sheria za Jamhuri ya Muungano na kwamba kila mtu ana haki ya kufuata utaratibu uliowekwa na sheria kuchukua hatua za kisheria kuhakikisha hifadhi ya Katiba na sheria za nchi.
Mheshimiwa Spika, moja ya sheria zilizotungwa ni Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge, ambayo inaeleza kitu gani Bunge linaweza kufanya na ambacho hawawezi kufanya na imeweka makosa ya jinai mle ndani. Niwakumbushe tu Waheshimiwa Wabunge kwamba tunazo
Kanuni za Bunge ambazo zinatungwa chini ya Ibara ya 89 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano kwa ajili ya kuendesha shughuli za Bunge hili.
Ibara hii ya 64 inasema hivi; “ Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katiba yanayolinda au kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika Bunge, Mbunge:
(a) Hatatoa ndani ya Bunge taarifa ambazo hazina ukweli;
(b) hatazungumzia jambo ambalo haliko kwenye mjadala;
(c) hatazungumzia jambo lolote ambalo linahusu uamuzi wa Mahakama au jambo lolote ambalo lilijadiliwa na kutolewa uamuzi kwenye Mkutano uliopo au uliotangulia na ambalo halikuletwa rasmi kwa njia ya hoja mahsusi.
Vilevile hatapinga uamuzi wowote uliofanywa na Bunge isipokuwa kwa kutoa hoja mahususi inayopendekeza kuwa uamuzi huo uangaliwe upya;
(d) Hatatumia jina la Rais kwa dhihaka katika mjadala au kwa madhumuni ya kutaka kulishawishi Bunge kuamua jambo lolote kwa namna fulani;
(e) Hatazungumzia mwenendo wa Rais, Spika, Mbunge, Jaji, Hakimu au mtu mwingine yeyote anayeshughulikia utoaji wa haki, isipokuwa tu kama kumetolewa hoja mahsusi inayohusu jambo husika.
(f) Hatamsema vibaya au kutoa lugha ya matusi kwa Mbunge au mtu mwingine yeyote, hatatumia lugha ya kuudhi au inayodhalilisha watu wengine.
Mheshimiwa Spika, nimeona niliseme hili ili kuwakumbusha Waheshimiwa Wabunge wajibu wetu kwamba shughuli zetu humu ndani zinaongozwa na masharti ya Katiba, zinaongozwa na masharti ya Kanuni tulizozitunga wenyewe, zinaongozwa na sheria. Tukifanya vile ndipo
tutaweza kutekeleza jukumu letu kwa ufanisi ipasavyo la kuisimamia na kuishauri Serikali katika utekelezaji wa majukumu yake.
Mheshimiwa Spika, wakati mjadala unaendelea hapa yamejitokeza mambo. Moja yamezungumzwa mambo ambayo yapo Mahakamani, naomba kushauri mambo yote ambayo yako Mahakamani, Katiba imekataza Ibara ya 30(2) ya Katiba imekataza, mambo yaliyopo Mahakamani, inalinda uhuru wa Mahakama na heshima ya watu walioko Mahakamani.
Mheshimiwa Spika, kesi ya mgogoro wa Chama cha CUF yapo Mahakamani. CUF wamepeleka Msajili wa Vyama vya Siasa Mahakamani na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Kwa hiyo ushauri kwamba mambo haya tusiyazungumze tena na mambo mengine. Pia mambo ya kutaja jina la Rais hovyo hovyo mambo hayo yote yamekatazwa hapa, kuwaudhi na yamewekewa utaratibu.
Waheshimiwa Wabunge wote tuna mamlaka lakini mamlaka haya yana mipaka. Ibara ya 100 ya Katiba imeshatafsiriwa na Mahakama Kuu ya Tanzania kwenye katika kesi ya Mheshimiwa Pinda na mimi ndiye niliyeendesha kesi ile, kwa hiyo tuna mipaka yetu. Tunapotekeleza wajibu
wetu tuzingatie mipaka hii, hakuna mtu ambaye yuko juu ya sheria na Mheshimiwa Mbowe amesema kwenye taarifa yake. Kwa hiyo, kama hivyo tunavyotambua hivi tufanye hivyo na naomba kushauri.
Mheshimiwa Spika, Kanuni hizi na sheria hizi, zimempa mamlaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwapeleka watu Mahakamani, sitaki kufika huko mimi, kwanza nawapenda sana, nawathamini sana. Hata Waziri Mkuu amesifu utendaji wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali uliohakikisha kwamba hizi kesi zilizokuwa zinawakabili zimekamilika mapema ili mrudi muwawakilishe wananchi wa majimbo yenu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hilo lazima mlielewe. Kipindi cha bajeti hii Wabunge nawashauri m-concentrate sana kwenye mambo yanayohusu wananchi wenu. Kule kuna shida nyingi watu wanataka maji, watu wanataka elimu, watu wanataka umeme, you would wish to concentrate on those important issues. Haya mambo mengine yaachieni Serikali itayashughulikia tu yenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo napenda kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mawaziri wote wanaohusika na Ofisi yake na timu yake kwa kazi nzuri wanayofanya, wameleta hapa hotuba nzuri sana inayoonyesha mambo makubwa ambayo Serikali hii imefanya mpaka sasa katika kipindi cha mwaka mmoja.Mungu aibariki Serikali hii, Mungu akubariki Waziri Mkuu,
Wabunge na wananchi wote. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuna mambo ambayo kimsingi hayapaswi kuletwa hapa, yamezungumzwa hapa mambo yanayohusu Usalama wa Taifa na mustakabali wa Taifa hili. Wabunge, tumetunga sheria sisi wenyewe hapa, tunayo Sheria ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1970 na tunayo Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1996. Juzi tumetunga sheria ya Whistleblower and Witness Protection, tumeweka masharti ni yapi ambayo yanaweza kuzungumzwa na yapi hayawezi kuzungumzwa na ni makosa ya jinai haya.
Ninawashauri Waheshimiwa Wabunge muda hautoshi, ningekuwa na muda ningesema yote haya, wazisome vizuri hizi sheria ni mambo gani ambayo hayapaswi kuzungumzwa kwa mustakabali wa Taifa hili.
Mheshimiwa Spika, haya mambo ya ulinzi na usalama yamewekewa utaratibu wake, hata Kamati yako, unayo Kamati ya Kudumu ya Ulinzi na Usalama, mnaona mambo yake yanazungumzwazungumzwa hapa hovyo hovyo? Halafu hatujajua kwamba hapa ni watu wa Usalama tu
kama alivyosema Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, hivi kila mtu anayebeba bunduki ni mtu wa mambo ya usalama, hatuwezi kufika kule.
Mheshimiwa Spika, kwanza kuna suala hapa nilitegemea Waheshimiwa Wabunge kwenye issue ya usalama watajikita sana kwenye mauaji ya viongozi wa Serikali kule Rufiji, watu wameuawa kule, and then tujiulize hii habari ya kutekateka hivi wameshatekwa watu wangapi? Katika
Serikali hii wametekwa wangapi? Hakuna hata watu wawili, ni mmoja. Kwa sababu aliyekwisha kutekwa mimi ninayemfahamu ni huyu mwanamuziki anayeitwa Mkatoliki. Huyu wa kwanza anayeitwa Ben Sanane so far haijulikani, ameondoka nchini, amejificha, yuko wapi, sasa
huwezi kusema ametekwa huyu. Halafu tutofautishe kuteka na kukamatwa na vyombo vya dola kwa ajili ya kuhojiwa.
Ukikamatwa na polisi ukaenda kuhojiwa huwezi kusema umetekwa.
Mheshimiwa Spika, naomba kulishauri Bunge lako Tukufu, kwenye suala hili we need to be so much serious and strict on enforcement of our rules. Hatuwezi tukafikia hatua, hivi kwanza mimi nashangaa, hili suala mtu mmoja na muda mfupi tu amepatikana na Waziri ameenda kuangalia pale mna-challenge, mlitaka achelewe kupatikana na huyo aliyesema Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, kazi zake zimetajwa kwenye sheria ya Baraza la Usalama wa Taifa. Vyombo vyote vya upelelezi viko pale, kama wamemwambia kwamba mwenendo wetu wa uchunguzi unaelekea tutampata hivi karibuni,
mnamhusishaje na utekaji nyara wa watu? Hili suala naomba lisikuzwe, linakuzwa nadhani lina sababu tatu za msingi.
Moja, inawezekana matukio haya wanataka kuyatumia watu wasio na nia njema na Taifa hili kufanya uhalifu, waseme kwamba kulikuwa na hii mipango, if you have any serious information about the crime… taarifa zote za uhalifu pelekeni kwenye vyombo vya dola. Hatuwezi
kufanya hivi. Huyu Ben Sanane hamuwezi kusema kwamba amekufa, Sheria yetu ya Ushahidi inasema ili uweze kuthibitisha kama mtu amekufa baada ya miaka mitano imepita na yule anayedai amekufa ndio ana jukumu la kwenda kuthibitisha hayo. Someni kifungu cha 117 cha Sheria ya Ushahidi, hatuwezi kufanya hapo.
Mheshimiwa Spika, jambo lingine ni kwamba watu wana vitendo vya uhalifu, labda wanahisi kwamba wakati wote watakamatwa na kuhojiwa inakuwa ni pre-emptive method.
Mheshimiwa Spika, yamezungumzwa hapa mambo ya uchaguzi Zanzibar, uchaguzi Zanzibar umeshapita. Uchaguzi wa Zanzibar
unatawaliwa na Katiba ya Zanzibar.
Mheshimiwa Spika, uchaguzi wa Novemba ulifutwa Kikatiba wakasema wanarudia mwezi wa tatu, 2016 ukarudiwa na sasa kuna Serikali kule haya yasizungumzwe hapa.
Mheshimiwa Spika, kuna mambo yanayozungumwa hapa ya mchakato wa Katiba Mpya. Mchakato wa Katiba Mpya tulitunga sheria, ipo Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, ipo Sheria ya Kura ya Maoni, hatua zote zimeshakamilika sasa kimebaki ni kiporo kwa mujibu wa ile sheria, muda muafaka utakaofika ambao mimi siujui mtaenda huko kwenye kupiga kura kama mtaamua hivyo. Kwa sababu kwanza ninyi wenyewe mlikuwa ni divided mara mlikuwa hamuitaki wengine mkasusia, eeh! Hata mimi nilivyosema tutunge sheria mkakataa wengine! Kwa hiyo, wakati muafaka hiyo mtapiga Kura ya Maoni we can not go back to the Constitution whatever.
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.