Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuchangia Mpango huu kwa kuunga mkono hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani.
Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali kwa Mpango huu uliowasilishwa Bungeni kuhakikisha unaendana na hali halisi ya ukusanyaji kodi na udhibiti wa mapato hayo. Mpango huu ujikite kuwezesha Mashirika ya Umma kama STAMICO, TPDC, TANAPA, TAZARA, ATC, TRL na kadhalika yajiendeshe kibiashara ili kuchangia katika bajeti ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mpango huu unapozungumzia miundombinu napenda kuona ni namna gani Serikali:-
(i) Itaboresha TAZARA.
(ii) Barabara ya kutoka Ifakara-Mlimba hadi Madeke Njombe ionekane kwenye bajeti hii ili wananchi ambao asilimia 90 ni wakulima na ni eneo linatoa mazao mengi kama mpunga, ufuta, ndizi, cocoa, miti, ng‟ombe na kadhalika. Jimbo hilo ni jipya ndani ya Wilaya ya Kilombero ambapo barabara hiyo ikijengwa itaunganishwa na Mkoa wa Njombe.
(iii) Jimbo la Mlimba halina barabara, halina Kituo cha Polisi, halina hospitali ya uhakika, halina Mahakama isipokuwa moja ndani ya Kata 16. Halina maji safi na salama ingawa lina mito mingi mikubwa ukiwemo na Mto Mpanga. Hali ya shule za msingi, awali ni tete sana, hakuna Chuo cha Ufundi wala Walimu wa kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi Mpango huu na bajeti hii ione namna bora ya kuingiza hela kwenye miradi ya maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilishashauri Bunge lililopita na naendelea kushauri namna bora ya kuhamasisha Watanzania kusaidia Serikali kukusanya kodi. Ni hivi, Dar es Salaam uwe mkoa wa majaribio ili ukifanikiwa uende nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, kila anayenunua bidhaa ahakikishe anapewa risiti ya TRA (electronic receipt) ambapo ataitunza na Serikali itaweka kiwango maalum cha fedha alizotumia na mwishoni mwa mwaka mtunza risiti huyo atarejeshewa kiasi fulani cha fedha alizotumia kama motisha. Ni muhimu Serikali ikajifunza toka nchi za wenzetu mbinu za ukusanyaji kodi. Haitoshi kusema tu, Watanzania daini risiti.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iliwezeshe Shirika la Umma STAMICO kwa kuwapa maeneo mapya ya kuchimba madini ya dhahabu na kadhalika ili ichangie pato la Taifa. Isiwe kama ilivyo sasa Shirika hilo la STAMICO linarithi migodi iliyoachwa na wawekezaji na kushindwa kuzalisha madini matokeo yake linapoteza pesa. Mfano, Mgodi wa tanzanite, Kiwira, Tulawaka na kadhalika, hata ukiangalia ni kiasi gani cha fedha zinazochangia kwenye bajeti ni sifuri, sana sana Serikali inazidi kulipa watumishi na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, Mpango huu umedhamiria kuboresha miundombinu ya barabara hivyo katika maboresho hayo kuwepo na msisitizo wa kujenga Barabara ya Ifakara-Mlimba-Njombe.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.