Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. ZAYNAB M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa rehema zake na kuendelea kutupatia amani kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali yangu kwa juhudi zake katika kuboresha miundombinu, huduma muhimu kwa wananchi wake, vyote hivyo vikiwa chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa. Kutokana na juhudi zote hizo tunaona jinsi gani Pato la Taifa lilipo ambapo ni asilimia saba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natoka Mkoa wa Pwani, tunashukuru kwa mkoa wetu ambao tumebahatika kuwa na viwanda ambavyo tayari vinazalisha na vingine viko kwenye hatua za ujenzi au taratibu za kuanzishwa. Pamoja na manufaa hayo kwa mkoa wetu kuna mambo
muhimu ambayo tunapaswa yapewe vipaumbele ili viwanda hivyo viweze kuwa na uzalishaji ambao hautakuwa na vikwazo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Pwani tuna tatizo kubwa la upatikanaji wa maji katika maeneo mbalimbali pamoja na neema tuliyopewa ya kuwa na mito mingi tena mikubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya barabara zetu sio nzuri, Wilaya ya Kisarawe imetenga eneo mahususi kwa ajili ya viwanda, lakini tatizo ni barabara. Hivyo basi naiomba Serikali inipe majibu ni vipi tutatokana na matatizo hayo ili kuweza kuvutia wawekezaji ambao wako tayari kuja
kuwekeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua ni kwa kiasi gani Serikali imejipanga kwa kuhakikisha ajira za vijana hasa kwenye viwanda vinazalisha na vinatarajiwa kuwa kuna baadhi wanatoa ajira lakini mshahara ni mdogo sana (shilingi 5,000) kwa siku. Hii nilishawahi kuuliza hapa Bungeni kwenye kipindi cha maswali na majibu. Mipango mizuri ndio faida ya Watanzania ambapo ni Serikali yetu inavyofanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme wa gesi utasaidia sana kupunguza gharama za uzalishaji viwandani, lakini pia utaratibu wa kupeleka umeme huo majumbani uongezewe speed.
Mheshimwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na pongezi kwa Mheshimiwa Jenista Mhagama na Naibu wake Mheshimiwa Antony Mavunde.