Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuipongeza hotuba ya Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa imegusa maisha ya wananchi wa aina zote katika nchi hii yetu ya Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Mheshimiwa Jenista Mhagama katika Wizara yake anafanya kazi kubwa na yenye tija kwa Taifa letu kwa ujumla na Naibu wake Mheshimiwa Antony Mavunde.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jimbo langu la Kibiti zipo changamoto nyingi katika suala zima la afya. Sina budi kushukru Serikali yangu inayoongozwa na Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kutuletea mradi wa BRF kwa kupata kila zahanati shilingi 10,000,000 kwa ajili ya kuboresha zahanati zetu na kununua baadhi ya vifaa vya tiba kama vitanda na vinginevyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kila penye mafanikio hapakosi changamoto, katika Jimbo la Kibiti changamoto kubwa katika idara ya afya ni moja ambayo ni upungufu wa watumishi, ikama ni 630 waliopo 152 upungufu ni 478; naomba Serikali yangu sikivu ya Chama cha Mapinduzi
watuangalie kwa jicho la huruma pamoja na upungufu wa watumishi lakini zipo changamoto zingine kama umaliziaji wa majengo, maboma yaliyoachwa kwa muda mrefu. Kituo cha Afya Kibiti kimezidiwa katika utoaji wake wa huduma, naomba iangaliwe kwa jicho la huruma kwani ndio inayobeba Kibiti kwa ujumla katika idara ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jimbo langu ka Kibiti zipo changamoto nyingi katika sekta ya kilimo kama maafisa ugani wapo wachache, kwa hiyo husababisha wananchi wangu wa Jimbo la Kibiti kushindwa kulima kilimo chenye tija. Hata hao wachache waliopo nao wana
changamoto ya uhaba wa vifaa vya kufanyia kazi kama magari na pikipiki, upatikanaji wa pembejeo kwa wakati nalo ni tatizo kubwa linalowakabili katika sekta hii ya kilimo katika jimbo langu la Kibiti, kwani pembejeo haziji kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushauri Serikali yangu sikivu ya Chama cha Mapinduzi hizi pembejeo ambazo tunaletewa kwa ruzuku naomba mfumo huu ubadilishwe kwa kuondolewa kodi ambazo si lazima ili pembejeo hizi ziwe kama vocha na kwa bei nafuu. Kuhusu mashamba darasa njia hii ni nzuri sana kwa wakulima wangu wa jimbo la Kibiti kuwapa elimu ili waweze kulima kilimo chenye tija; aidha, stakabadhi ghalani ni mfumo ambao nao katika uuzaji wa mazoa ni mzuri lakini unachangamoto kubwa kama chama kikuu cha CORECO – Pwani kina matatizo makubwa na moja ni kufanya minada kiujanja, pili kuchelewesha malipo ya minada na vilevile vyanzo vya msingi navyo ni tatizo tuna kila sababu ya kupitia upya mfumo huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu, sina budi kuishukuru Serikali yangu kwa kuanzisha elimu bure. Lakini kila penye mafanikio hapakosi changamoto, moja upungufu wa walimu, vyumba vya madarasa, vyumba vya walimu na baadhi ya maeneo watoto hutembea umbali mrefu
kwenda kwenye shule. Katika jimbo langu la Kibiti kuna maeneo ambayo yapo kwenye delta, walimu wanafanyakazi kwa hali ngumu kabisa. Naomba wafanyakazi hawa wa maeneo haya ya delta wapewe hata posho ya kujikimu ya mazingira magumu.
Mwisho namshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Elimu mama yetu Joyce Ndalichako kwa kufanya ziara katika jimbo langu la Kibiti hasa maeneo ya delta, maeneo ya Nyamisati, Salale, Mfisini na tunashukuru sana kwa kutuletea pesa za ujenzi wa mabweni shule ya sekondari Nyamisati shilingi 261,000,000 na Mtanga delta shilingi 256,084,461.25 tunashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika sekta hii ya miundombinu kama barabara ya Bungu - Nyamisati tunaomba barabara ijengwe kwa kiwango cha lami kwani kipindi cha mvua huwa inapitika kwa taabu sana ukizingatika barabara hii inatumika kwa majimbo
mawili, wananchi wa Kibiti na Mafia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ujenzi wa gati la Nyamasati nalo ni muhimu sana kwa wananchi waishio maeneo ya delta. Kwa ujumla barabara ya kutoka Muhoro – Mbwera barabara hii nayo ni muhimu sana kwa wananchi waishio maeneo ya Mbuchi, Mbwera, Kipoka Maparoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.