Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nichukue fursa hii kuipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu kwa utekelezaji na usimamiaji mzuri wa mipango ya Serikali iliyoandaliwa kwa kuzingatia Ilani ya CCM. Hata hivyo napenda kuchangia katika maeneo yafuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama; Ofisi ya Waziri Mkuu itambue kuwa Wilaya ya Mkalama ni moja kati ya Wilaya mpya na huduma za mahakama zinazopatikana katika Wilaya ya Iramba (Kiomboi) na hivyo kusababisha usumbufu mkubwa na haki kupotea kwa wananchi wa
Wilaya hii. Ninaomba katika bajeti ya mwaka 2017/18 Wilaya ya Mkalama ijengewe Mahakama ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Mkalama wanajihusisha na kilimo kinachotegemea mvua za msimu lakini kwa bahati mbaya mvua hizo zimenyesha chini ya wastani katika msimu wa mwaka 2016/2017 unaomalizika sasa na ofisi ya Waziri Mkuu imefanya tathimini na kubaini
kwamba Halmashauri 55 zimeathirika na ukame. Hivyo napenda Ofisi ya Waziri Mkuu itambue na kuingiza Wilaya ya Mkalama katika Halmashauri zilizoathirika na ukame kwani kata zifuatazo mvua haijanyesha, Mpambala, Mwangeza, Gemenga na Mafongo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sera ya madini inatoa mwongozo wa usimamiaji vizuri wa sekta hii lakini uzoefu unaonyesha kuwa uratibu wa sekta hii ikiwemo utaratibu wa utoaji leseni hauendani na sera iliyopo mfano. Leseni za kuchimba madini ya gypsum katika eneo la Dominiku -
Mkalama bila wananchi kuhusishwa na hivyo kuzua migogoro kati ya wananchi na waliopewa leseni. Tunashauri Serikali ichukue hatua na kufuta leseni hizo au kuhakikisha wananchi wanapata fidia stahiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu migogoro ya mipaka na ardhi napenda kuweka bayana kuwa migogoro ya mipaka kati ya Mkoa na Mkoa na Wilaya kwa Wilaya haijapatiwa ufumbuzi ama kama zipo juhudi basi zinaenda kwa mwendo wa kinyonga yaani polepole. Tangu niingie
Bungeni nimetoa taarifa za kuwepo mgogoro katika maeneo yafuatayo; mgogoro wa Singida - Manyara na Singida – Simiyu. Migogoro hii ya mipaka inasababisha migogoro na mapigano kati ya Wilaya zifuatazo; Mkalama - Mbulu, Eshijeshi - Iranoto, Mkalama - Mbulu, Singida A – Singida B, Mkalama - Singida Vijijini, Mkarama - Iramba na Mkalama - Nyahaa – Simiyu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tume iliyoundwa naamini haina taarifa hizi na wapo wananchi wameumizwa kwa mapanga. Nashauri suala hili litolewe maagizo maalum lishughulikiwe.