Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa hotuba nzuri ya bajeti imegusa kila nyanja ya maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu, pamoja na kazi inayofanywa na Serikali kwenye sekta hii zipo changamoto nyingi lakini niiombe Serikali kuja na mpango mahsusi wa kuondokana na madeni ya walimu. Niiombe Serikali kuja na mpango wa teaching allowance ili iwe motisha kwa walimu
kama inavyotoa kwa viongozi yaani responsibility allowance.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maji; naishukuru Serikali kwa kuendelea kuwajali wananchi wa Jimbo la Singida Mjini. Naomba nizungumzie miradi ya vijijini 10 inayofadhiliwa na Benki ya Dunia changamoto kubwa inayojitokeza katika Jimbo la Singida Mjini ni kuwa miradi yote imekamilika
akini wananchi hawapati maji tatizo kubwa ni kwamba umefanyika uchakachuzi mkubwa katika ujenzi wa miundombinu ya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Singida Mjini tumejaliwa rasilimali ya vyanzo vya umeme:-
(i) Umeme wa upepo na makampuni mawili yaliyojitokeza ni:-
(a) Power pool
(b) Wind East African Company.
(ii) Umeme wa jua (solar power) na kampuni ya Synohydro ya China wamejitokeza kuzalisha umeme huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba TANESCO ipunguze urasimu katika kutoa PPA na pia TANESCO inapaswa kuyaacha makampuni kuzalisha umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shilingi milioni 50 kila kijiji, naiomba Serikali yafuatayo; kwanza isomeke shilingi milioni
50 kila kijiji na kila mtaa ili kutoa fursa kwa majimbo ambayo hayana vijiji bali ni mitaa kama Singida Mjini na pia fedha hiyo itoke mapema.