Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Hamadi Salim Maalim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kojani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. HAMAD SALIM MAALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kutupa uwezo walau wa kukamata kalamu na kuandika haya machache.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianzie mchango wangu wa bajeti hii ya Ofisi ya Waziri Mkuu katika ukurasa wa 10 wa kitabu chake kwenye mada ndogo ya siasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kifungu hiki tumeelekezwa kuwa hali ya siasa nchini ni shwari ambapo ukiangalia kwa umakini unaona kuwa kauli hiyo haina ukweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mara baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2015 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alizuia Vyama vya Siasa kutofanya kazi zake kama ilivyoelekezwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Vyama vya Siasa vina viongozi wake waliochaguliwa kwa mujibu wa Katiba zao ukiachia mbali na Wabunge. Unapomruhusu Mbunge kufanya mikutano ya hadhara katika Jimbo lake lakini ukamzuia Mwenyekiti au Katibu Mkuu kutofanya mikutano katika maeneo yaliyomo ndani ya nchi ni kinyume na Katiba na kwa maana hiyo
hatuwezi kusema kuwa hali ya siasa ni shwari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la demokrasia ambalo limeelezewa ukurasa 11 wa kitabu cha bajeti ni kweli kwamba nchi yetu inajenga demokrasia lakini demokrasia kama tunavyojua ina uwanja mpana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, demokrasia ni pamoja na
uhuru wa watu wa kutoa maoni yao, uhuru wa vyombo vya habari, uhuru wa kukosoa na kukosolewa kwa Serikali iliyo
madarakani na mengineyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii nchi hii inashuhudia jinsi raia wanavyoishi kwa woga na hofu, kosa ni kuisema Serikali. Vyombo vya habari navyo vinashindwa kufanya kazi zake kwa ufanisi huku vikijua kwamba kukosoa mamlaka ya dola ni kujitafutia balaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vielelezo vyote hivyo ni uthibitisho tosha kwamba suala la demokrasia tunalihubiri tu, lakini kivitendo halipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la Msajili wa Vyama vya Siasa nchini ni kwamba tunaelewa fika kwamba yeye si muamuzi wa kuwachagulia vyama vya siasa viongozi wa kuwaongoza. Ofisi hii ipo kwa mujibu wa Katiba kwa lengo la kusajili vyama vya siasa na pia kuvishauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Msajili wa Vyama vya Siasa hana mamlaka ya kuwachagulia wala kuwapangia vyama vya siasa viongozi ambao kwa mujibu wa Katiba za vyama hivyo si viongozi tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vyama vya siasa vinaongozwa na Katiba zao, lakini mbali na Katiba zao, pia kuna Katiba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba Msajili wa Vyama vya Siasa atuelekeze ni Katiba ipi kati ya hizo tatu inayotoa uhuru wa kiongozi kujiuzuru na baadaye akarejea kwenye nafasi yake hiyo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na hayo ambayo Lipumba alijiuzulu na baadaye Ofisi ya Msajili ikamtambua kama Mwenyekiti halali wa chama, tunamuomba Msajili wa Vyama kama vile ambavyo anaheshimu maamuzi ya vyama vingine kwani vyote ni sawa kwa matakwa ya Katiba zao.