Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana hotuba ya Waziri Mkuu kwa sababu imetaja maeneo ambayo Serikali inafanya kazi zake. Kwa kuwa maji ni muhimu kwa maisha ya binadamu Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba sana kuishauri Serikali kufanya ukarabati wa miundombinu ya maji ambayo imeharibika na wananchi wanashindwa kupata maji safi na salama. Jimbo la Mufindi Kusini tuna tatizo kubwa la maji Serikali iliweza kujenga matanki ya kutosha katika Jimbo la Mufindi Kusini lakini matanki hayo hayafanyi kazi sababu ya
miundombinu kuharibika katika Kata za Nyololo, Idunda, Itandula, Mtambula, Ihomasa, Igowole, Kibao na Sawala. Wananchi wanapata shida kubwa ya maji kutokana na kuwa na matanki ambayo hayawezi kuhifadhi maji kutokana na miundombinu mibovu. Nitashukuru sana kama Serikali itafanya ukarabati wa miundombinu hiyo ili wananchi wa Jimbo la Mufindi Kusini waondokane na tatizo hili la maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Umeme, naiomba sana Serikali kupeleka umeme katika Jimbo la Mufindi Kusini vijiji vingi bado havina umeme. Kata ya Idunda ina vijiji vitatu navyo havina umeme. Kata ya Itandula vijiji sita havina umeme, Kata ya kiyowela vijiji vinne havina umeme, Kata
ya Maduma vijiji vitatu havina umeme Kata ya Kasanga vijiji vitatu havina umeme, Kata ya Nyololo vijiji vinne havina umeme. Jumla ya vijiji 48 katika jimbo la Mufindi Kusini havina umeme. Naibu wa Nishati na madini alikuja na kuahidi kuwa Serikali itapeleka umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Afya, naomba sana Serikali kujenga kituo cha Afya katika Kata ya Makungu, Idete, Kiyowela, Luhanga, Mtambula, na Mtwango. Katika kata hizi wananchi wanapata shida kubwa ya kukosa vituo vya afya. Pia tuliomba gari la wagonjwa ambalo litahudumia kata tatu, Makungu, Kiyowela na Idete. Bado hilo gari hatujapata na Serikali iliahidi kutoa hilo gari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.