Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, naomba nianze kwa kupongeza Serikali kwa kazi nzuri inayofanya kwa kupitia Mheshimiwa Waziri Mkuu, nampongeza sana kwa kufika na kutatua changamoto sugu jimboni na Mkoani Manyara. Pamoja na pongezi hizi tunazo changamoto na ahadi tulizopewa na Serikali kupita viongozi wetu wa Kitaifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Miundombinu; tunaomba kujengewa barabara ya kutoka Karatu –Mbulu, Haydom Singida/Sibiti maana inasaidia ikiwa itajengwa kwa lami. Barabara hii inapita katika majimbo matano na hata itasaidia sana wananchi kufika katika Hospitali ya Kilutheri
ya Haydom ili kupata matibabu na pili itasaidia wananchi kiuchumi katika maeneo yetu.
Mheshimiwa Mwenyekjiti, kupandishwa hadhi hospitali ya Kilutheri ya Haydom iwe ya Kanda kama ulivyoahidi. Jambo hili la kupandishwa hadhi itasaidia sana kuhudumia jamii inayozunguka. Mikoa ya Simiyu, Manyara, Arusha, Singida, Tabora na sehemu ya Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna tatizo kubwa la miradi ya maji ambayo imekwama kutokana na kutopata fedha kwa wakandarasi. Hoja, mradi wa maji Hydom- Tumati, tunaomba Serikali ifanye mkakati wa kuwasaidia wakandarasi. Mifugo/Kilimo katika jimbo langu kuna wizi wa mifugo ambao umepelekea kufariki kwa kuuawa zaidi ya wananchi wanne na zaidi ya mifugo 500 kuibiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali iimarishe usalama katika Bonde la Yaeda Chini/Eskesh Kilimo. Tunaomba sasa mbegu na mbolea zinazotolewa kwa wakulima zije kwa muda muafaka yaani kabla kunyesha mvua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, afya ipo katika ilani ya CCM kujenga zahanati kila kijiji. Naomba nitoe ushauri ni bora Serikali kutoa maelekezo mahususi kujikita katika kujenga kituo kimoja cha afya kila Halmashauri kwa mwaka wa fedha ili baada ya miaka mitatu tutakuwa tuna vituo ziadi ya 500 hapo ndipo tutaona matokeo ya haraka katika Sekta ya Afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, nawapongeza sana, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri, Mheshimiwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kwa kazi nzuri.