Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napongeza sana kwa hutuba nzuri sana. Pili naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia haya yafuatayo:- CDA ni chombo cha Serikali Kuu na chombo hiki kipo ndani ya Manispaa ya Dodoma, Manispaa ya Dodoma ni chombo cha mamlaka ya Serikali za Mitaa. CDA wanapima viwanja na kuchukua mapato ya ardhi kodi ya ardhi ambayo ipo chini ya Manispaa ya Dodoma na Manispaa wanapima viwanja na kuchukua kodi ya viwanja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Mheshimiwa Waziri Mkuu huu sio mgogoro kati ya CDA na Manispaa ya Dodoma kwa kuwa Kisheria ardhi yote ni mali ya Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma na ndiyo wenye haki ya kupima viwanja na kupata kodi ya viwanja (ardhi) na sio CDA. Sheria
iliyoanzisha CDA iangaliwe upya, CDA ilianzishwa kwa ajili ustawishaji wa Makao Makuu Dodoma na tayari Makao Makuu Dodoma yameanza.