Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi kubwa anayoifanya, nampongeza Mheshimiwa Waziri Jenista na mdogo wangu Mheshimiwa Mavunde kwa kazi nzuri wanayomsaidia Mheshimiwa Waziri Mkuu, mambo
yanakwenda vizuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya pongezi zangu naomba nianze kuchangia katika kilimo cha tumbaku ambacho wakazi wa Mkoa wa Tabora ndiyo zao la kiuchumi kubwa tunalolitegemea katika mkoa wetu. Baada ya malalamiko mengi ya Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa
Waziri Mkuu kwa usikivu mkubwa sana ameanza sasa kufuatilia kero mbalimbali na kutatua changamoto zilizopo katika zao letu la tumbaku.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, hongera kwa kazi kubwa unayoifanya sasa wananchi wa Tabora, kwa kuwa walikuwa wanahisi kwamba korosho na wewe unatoka huko sasa tunaamini ni mchapakazi na kero za tumbaku zitakwisha na sasa tunakoelekea mkulima wa tumbaku atapata faida ya zao hili la tumbaku ambalo analilima. Mheshimiwa Waziri Mkuu unajua tumbaku ikisimaiwa sawasawa ni zao ambalo linaingiza pato kubwa kwa nchi yetu, itasaidia katika maeneo mbalimbali ya kutatua kero za wananchi wetu kwa ujumla katika nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, yapo machache ambayo tunataka Mheshimiwa Waziri Mkuu utusaidie ili zao hili liendelee kumnufaisha mkulima wetu. Zipo tozo mbalimbali ambazo mkulima anakuwa-charged zinapunguza faida yake katika zao zima la tumbaku. Tunaomba tozo hizi zipungue zibakie tozo za msingi ili kumwondolea mkulima mzigo mzito aliokuwa nao. Tunataka tupate bei nzuri na ili kupata bei nzuri ni lazima sasa tuangalie pia masoko mengine ya kuweza kupata wanunuzi wa tumbaku ili zao hili sasa liweze kuleta tija kwa mwananchi wa Mkoa wa Tabora. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lipo suala dogo pia kuhusu hawa wakulima (independent farmers) ambao tuliwaambia warudi kujiunga na ushirika, wamekubaliana na wazo hili wameshajiunga na vyama vya ushirika, tunaomba sasa na wenyewe wasaidiwe ili kuwasaidia katika kilimo chao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia wakati tunaangalia zao la tumbaku, sisi Tabora tunarina asali nzuri sana, tunarima asali nyingi, juhudi hizo zinazoelekezwa katika kutatua changamoto za mazao mengine naomba tuliangalie zao la asali pia katika kuboresha mazingira yake,
kwanza katika kuliandaa zao lenyewe na kurina asali hiyo mwisho wa siku kuitafutia soko litakalomsaidia mkulima wa asali katika Mkoa wa Tabora. Asali ni dawa, asali ni kitu ambacho kinasaidia katika maeneo mengi na vilevile inaongeza mapato kwa wananchi wetu wa Mkoa wa
Tabora na maeneo mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee tatizo la maji lililopo katika Mkoa wa Tabora sana katika Jimbo langu la Igalula. Tunapongeza juhudi za Serikali katika kutatua changamoto za maji katika Mkoa wetu wa Tabora, kwa sasa tunatarajia kupata maji kutoka Ziwa Victoria.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema huko nyuma, mradi huu wa kuleta maji toka Ziwa Victoria katika Jimbo langu la Igalula hatumo katika programu ya kuleta maji ya Ziwa Victoria, baadhi ya maeneo mengine wanapata maji hayo sisi tumekubaliana na hilo, tunajua Serikali itatuangalia baadae, kwa sasa tunaomba Serikali iangalie njia mbadala za kutatua kero za kupata maji katika Jimbo letu la Igalula ikiwemo kuchimbiwa visima, kuchimbiwa malambo kwa sababu mazingira yanaruhusu kuweza kuchimba mabwawa na kuweza kutatua kero za maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana tuliambiwa tutafanyiwa usanifu katika Kata ya Goweko tuna bwawa moja kubwa na Kata ya Loya, lakini sijaona chochote ambacho kimefanyika, tunaomba Serikali iangalie. Tumekosa mradi wa maji ya Ziwa Victoria basi tuweze kuangaliwa
kupata maji katika maeneo mengine.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, najua bajeti mwaka huu sio nzuri sana kuweza kutekeleza miradi yote ya maji lakini nakumbuka tulijaribu kuishauri Serikali namna ya kupata pesa za kugharamia miradi ya maji katika vijiji vyetu. Tulishauri hapa kwamba tuongeze hata shilingi 100 katika bei ya petroli ili hela hizo ziende kwenye mfuko wa maji ziweze kutatua kero za maji katika vijiji vyetu, Serikali haijakubaliana na wazo hilo. Naomba sasa Serikali ikubali tuongeze shilingi 100 katika
bei ya mafuta ili tuweze kutengeneza mfuko wa maji utakaosaidia kutatua kero za maji katika maeneo yetu, tumtue mama ndoo kijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mama anateseka kupata maji kilometa zaidi ya 10 hadi 15, mwisho wa siku mama huyu anarudi apike chakula, mama huyu tunashindwa kumsaidia. Tunaomba tuweze kufanya hili ili kuweza kusaidia kutatua kero ya maji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nisemee kidogo suala la barabara. Wakati nataka kuchangia katika barabara naomba nitoe pongezi kwa Serikali kusikia kilio chetu cha
barabara ya Itigi – Tabora, kipande cha Chaya – Nyahua cha kilometa 85 ambacho kimekuwa ni kero kubwa sana kwa wasafiri wanaokwenda Kigoma, Mpanda na Katavi, pamoja na wasafiri wanaokwenda Tabora. Kipande kile kikitengenezwa wasafiri wa Kigoma badala ya kuzungukia Nzega na Igunga watapunguza kilometa zisizopungua 140 kufika Tabora na maeneo mengine. Tumepata pesa toka Kuwait Fund nina hakika kabisa tutatengenezewa barabara hii, tunashukuru sana kwa kusikia kilio cha Wanatabora na maeneo mengine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niliomba kipande changu cha barabara kipandishwe hadhi kutoka Buhekela kuja Miswaki kuja Loya kwenda Iyumbu. Barabara hii ni muhimu sana inaunganisha majimbo manne ya uchaguzi, Jimbo la Igunga, Jimbo la Manonga, Jimbo la Igalula na Jimbo la
Singida Vijijini, inaunganisha Wilaya tatu, Wilaya ya Igunga, Wilaya ya Uyui na Wilaya ya Singida Vijijini. Pia inaunganisha mikoa miwili ya Tabora na Singida. Kuna kilimo kikubwa sana cha mpunga kule, barabara hiyo mvua ikinyesha katika kipindi cha miezi minne haipitiki, tunaomba Serikali itusaidie katika hili kama walivyosikia barabara ya Chaya nina hakika na barabara hii tutasaidiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la elimu. Ninaipongeze Serikali kwa namna inavyoboresha upatikanaji wa elimu sasa, elimu bure baadhi ya watu wanasema haijaleta mafanikio makubwa, lakini kila jambo lazima liwe na mwanzo, mwanzo lazima kuna changamoto nyingi, tumekutana na changamoto nyingi Serikali itazifanyia kazi. Kiukweli wananchi wetu waliokuwa wanashindwa kupeleka watoto wao shule sasa wanapeleka watoto shule na ushahidi ni kwamba shule hizo madarasa yamejaa tunaelekea kupata changamoto ya kujenga vyumba vya madarasa. Kwa hiyo, Serikali ijipange kuboresha kupata madarasa pia napongeza tumetengeneza madawati ya kutosha, mpaka sasa madawati yanawekwa nje, hili lazima tupongeze. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lazima tuboreshe mazingira ya ufundishaji, maslahi ya walimu ni lazima tuyaboreshe, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge pale madai ya walimu ni lazima tuyaangalie. Tunapoboresha maslahi yao, mazingira ya kufundishia pia lazima tuyaboreshe kwa maana ya kujenga nyumba za kuishi walimu katika maeneo yetu, walimu wanapata taabu pa kukaa, wanaondoka kufundisha vijijini kwa sababu hakuna nyumba za kuishi. Lazima tutengeneze mkakati mzuri wa kuhakikisha kwamba katika kuboresha elimu na nyumba na maslahi ya walimu ni jambo la msingi sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika elimu pia naomba niseme jambo moja, vijijini kuna maeneo ni mbali zinapopatikana shule za msingi. Tumeanza kuhamasisha kujenga satellite schools ambazo zinasaidia watoto badala ya kutembea kilometa zaidi ya 20 kwenda kufuata shule
mama tumeamua kuzijenga ili ziweze kutatua changamoto ya elimu, lakini bahati mbaya sana Wizara ya Elimu haitusaidii, wananchi wanajenga shule hizi katika wakati mgumu sana, nyingine zimetimiza vigezo zaidi ya asilimia 70 lakini kigezo kikubwa sana ni umbali kutoka katika satellite kwenda kwenye shule ile mama, zaidi ya kilometa 20 mtoto anatembea, hii inasababisha mtoto anakataa tamaa ya kwenda shule, wasichana wadogo wanabakwa njiani wanakatishwa masomo, tunasema tunataka kuzuia mimba za utotoni lakini kwa kuzuia kusajili satellite schools hizi tunaweza tukasababisha pia mimba za utotoni kwa hawa watoto kubakwa njiani wakati wanakwenda kutafuta shule.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba zile shule ambazo tumesema zisajiliwe Mheshimiwa Waziri, tunatoka huko mazingira ni magumu, wananchi kutokana na hali ngumu hii tunawachangisha pesa tunajenga shule zile, zingine zimefikisha vigezo at least aslimia 70 na kuendelea, tunaomba zisajiliwe. Kikubwa ni kusaidia nguvu za wananchi ambazo wanazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya yetu ya Uyui ni Wilaya mpya, tunajenga…
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana.