Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza leo kwa sababu ni mara ya kwanza kuongea katika Bunge hili la Kumi na Moja, nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mtoa haki. Pili, namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuniona, kwa kutambua mchango wangu na kunirejesha Bungeni. Namshukuru sana, namshukuru sana, namshukuru sana! (Makofi)
Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu nitachangia kitu kimoja tu. Nitachangia ukurasa wa 21 Kifungu cha 31 kuhusu kilimo. Hotuba yangu itakuwa ni ndefu, kwa hiyo, nusu nitaongea kwenye hotuba ya Waziri Mkuu sitamaliza, nusu nitaongea kwenye Wizara ya Kilimo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wizara ya Kilimo na nitaongea kitu kimoja kuhusu tangawizi. Leo naiongea tangawizi kwa mapana yake. Watu wanaweza wakajiuliza, hii tangawizi ni nini? Wengine hawaelewi tangawizi ni nini. Tangawizi ni zao la viungo (Spices), lakini tangawizi ni
malighafi ya kutengeneza dawa za binadamu, kutengeneza cosmetics, nikiwa na maana ya vipodozi, vinywaji na vitu vingine vidogo vidogo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niigawe hii tangawizi katika mafungu matatu; kwanza nitaiongea tangawizi kiulimwengu, kwa Afrika na mwisho nitaiongea kwa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, duniani hapa, ulimwenguni, nchi bora tano zinazoongoza kwa kulima tangawizi ya kwanza ni India, lakini India inaongoza kwa kulima tangawizi duniani na inayoongoza kwa kutumia tangawizi duniani. Nchi ya pili ni China; ya tatu ni Nepal; na ya nne ni Nigeria. Ni nchi ya Kiafrika hii na inalima tangawizi kweli na ina-export tangawizi kwa wingi mno.
Waheshimiwa Wabunge, kama mnasoma vitabu vya kilimo, utakuta kwamba Nigeria imekuwa inategemea zao la tangawizi kwa export mpaka ilipofika mwaka 1960 ndipo ilipogundua mafuta, ikawa mafuta yako juu kwa tangawizi. Sisi huku, nikisema tangawizi, watu wanasema, “huyu naye na tangawizi!” Tangawizi ni zao zuri sana na lina export nzuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi ya nne ni Nigeria kwa hiyo ni ya kwanza kwa Afrika. Nchi ya tano ni Thailand. Nisiishie hapo kwa upande wa ulimwengu, twendeni tuangalie nchi zinazo- export tangawizi kwa wingi. Sasa kwa sababu India inalima tangawizi kwa wingi, lakini anaiconsume yeye mwenyewe sana. Ameshindwa kuwa wa kwanza kwenye ku-export. Nchi ya kwanza inayo-export tangawizi kwa wingi ni China; ya pili inakuja kuwa India; ya tatu, watu hawataamini, Nigeria ni giant number three kwa ku-export tangawizi; ya nne inakuwa ni German na Netherland.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nirudi Afrika. Nilitaka kutoa picha ya tangawizi na ulimwengu kidogo tu. Twende Afrika sasa. Nigeria inaongoza kwa kulima tangawizi Afrika. Nigeria inajipambanua kwamba kwa nini inaongoza kulima tangawizi na ku-export? Inasema kwa nini inafanya hivyo? Kwa nini imeweza? Inasema ina ardhi kubwa sana yenye rutuba; inasema, ina mvua za kutosha na mito isiyokauka, lakini inasema ina hali ya hewa nzuri, ndiyo maana imeweza kuwa na comperative advantage upande wa tangawizi kuliko nchi zote za Afrika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Nigeria imefika hapo, kwamba ina-export tangawizi inapeleka USA, Europe, Morocco na nchi nyingi tu. Kitu cha ajabu, yenyewe kama Taifa inakubali kwamba wakulima wakubwa wa tangawizi kwa Nigeria asilimia 40 ni wanawake. Wanawake wa Nigeria ndio walioshika mashamba makubwa ya tangawizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hali ya hewa ya Nigeria, nakubali ni nzuri; ardhi ya Nigeria, nakubali ni nzuri. Ile hali ya hewa ya Nigeria ambayo imeruhusu kulima tangawizi, ipo Tanzania! Ukisema mvua, Tanzania tuna mvua; ukizungumza mito isiyokauka; tunayo, twende tuone mfano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda Mkoa wa Ruvuma kuna mvua ya kutosha; Mkoa wa Njombe una mvua ya kutosha; Mbeya ina mvua ya kutosha, Rukwa na kigoma; Tanzania haina maana kwamba hatuna sehemu zenye hali ya hewa nzuri, haina maana kwamba hatuna mito ya
kutosha, haina maana kwamba hatuna ardhi ya kutosha. Kwa nini wenzetu wamefanikiwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Nigeria imethamini zao la tangawizi, imekwenda imesimama imara kwenye zao la Tangawizi, lakini kwetu sisi, Kipare tuna methali inasema, “Ng’ombe kuramoshe ukuhundue.” Ina maana Ng’ombe anajipeleka mwenyewe machungani, anajirudisha
mwenyewe. Wakulima wa Tanzania wanaolima tangawizi wako wenyewe. Serikali haijasimama imara ikalishika hili zao, ikatayarisha project maalum ya ku-study hili zao la tangawizi na ikasimama imara ikatafuta hili zao wapi tutalilima? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hatuwezi kuwa na Tanzania ya viwanda kama hatutakuwa na kilimo bora, hatuwezi. Itakuwa tunasema, Tanzania ya viwanda, Tanzania ya viwanda! Ni lazima tukaboreshe kwanza kilimo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hili nitaliongea miaka mitatu na nusu. Naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge, Jimbo langu sasa ni Tangawizi. Nitazunguka nchi nzima kuhakikisha naboresha kilimo cha Tanzania na nina uhakika Serikali mtaniunga mkono kila siku. Ofisi nitakayokwenda
kuiona mimi ni Ofisi ya Wizara ya Kilimo. Nitakwenda, nitashauri, nitapita, nitakwenda, nitarudi. Serikali naomba zao la tangawizi hebu tuliangalie, tukae, tuandike project, tutafute wenzetu wa Nigeria, twende tukai-visit Nigeria; siyo lazima mtulipie nauli, tutalipa wenyewe. Mimi nitakwenda Kaduna nikajue kwa nini Kaduna wanalima tangawizi kwa wingi? Nitafanya hiyo kazi. Hatuwezi kuzungumza suala la viwanda kwa nguvu, tutafika, lazima tujenge viwanda; kilimo kiko wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumze ukweli; zao la tangawizi ndugu zangu, ukiona Muhindi, ni very aggressive huku duniani; Mchina ni very aggressive; MNigeria ni very aggressive; kwa nini haya Mataifa matatu yanasimama kulima tangawizi? Wanajua faida yake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa leo, naomba niishie nusu ya hotuba yangu. Wizara ya Kilimo, naendelea na zao la tangawizi na nitachangia kwa maandishi, nitamletea Mheshimiwa Waziri Mkuu. Kabla sijamaliza, nirudi niseme naipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Nilikuwa nje kwa mwaka mmoja na miezi kadhaa. Nilikuwa nawaangalia mnavyochacharika, Serikali mnafanya kazi sana, lakini naomba mwongeze nguvu kwenye kilimo cha Tanzania. Ni lazima tuondoke hapa tulipo. Tutaondoka tu kama tutakuwa na viwanda vya uhakika. Hilo linawezekana iwapo tutashirikiana wote tena tukitaka kujenga nchi vizuri, tushirikiane bila kujali itikadi zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.