Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Awali ya yote nipende kumshukuru sana Mungu kwa ajili ya kila mmoja wetu aliyeko hapa ndani kwa sababu ni wengi walitamani kuwepo hapa siku ya leo lakini wameshindwa, si kwamba sisi ni wema sana ila ni kwa
rehema tu za Mungu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nitumie fursa hii kutoa pole nyingi sana kwako Mheshimiwa Naibu Spika, Spika wa Bunge lakini pia kwa Wabunge wote kwa kuondokewa na mpendwa wetu, Mheshimiwa Dkt. Elly Macha. Kundi la watu wenye ulemavu tumepoteza, Tanzania na duniani kote, kwa sababu ikumbukwe mwaka jana Mheshimiwa Dkt. Elly Macha alichaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Wasioona Duniani.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, mambo aliyoyafanya katika kipindi hiki cha mwaka mmoja ni mengi na yanafahamika.
Mheshimiwa Jenista Mhagama pongezi nyingi, Mheshimiwa Dkt. Possi tulikuwa naye na hata sasa hivi ametuachia alama kwamba hata kwenye upitishaji wa sheria mbalimbali watu wenye ulemavu wanaonekana; kwenye uundwaji wa bodi tunaona watu wenye ulemavu tunaonekana, kwa hiyo Mheshimiwa Dkt. Possi ameacha alama. Nimpongeze Mheshimiwa Mavunde, amekuwa pamoja na sisi kipindi hiki
ambacho Mheshimiwa Dkt. Possi ameondoka, amekuwa ni msikivu sana. Kwa hiyo naomba niwapongeze sana kwa utendaji wao.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia napenda niishukuru sana Serikali kwa kupatia mwarobaini tatizo la vifaa vya kujifunzia na kufundishia, kilikuwa ni kilio cha watu wenye ulemavu ama watoto wenye ulemavu lakini Serikali imetoa mwarobaini wake kwa kutatua tatizo hili la vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa asilimia kubwa. Lakini pia katika bajeti ya mwaka huu yapo mambo mengi ambayo yameongezeka ambayo kwa bajeti ya mwaka jana hayakuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaona kuna suala zima, ukisoma kwenye randama ndipo unaona hivi vitu. Wakati napitia randama ndipo nilipoona; kuna suala zima la ununuzi wa madawa, mambo ya ununuzi wa kuni kwa habari ya vyuo vya watu wenye ulemavu, lakini pia bajeti ya chakula imeongezeka kutoka milioni 38 ya mwaka wa fedha huu tunaoumaliza na kufikia milioni 126 kwa mwaka huu wa fedha ambao ndio tunapitisha sasa hivi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia napenda niipongeze sana Serikali kwa kuwakumbusha tena wakuu wa mikoa kwa habari ya uundwaji wa kamati za watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya kijiji mpaka mkoa. Kwa nini nasema kuwakumbusha tena; Serikali ilishatoa agizo, nakumbuka
ilikuwa Januari mwaka huu wakati likijibiwa swali langu la nyongeza, Serikali iliagiza kwamba hizi kamati ziundwe. Sasa ushauri wangu katika hili kuwakumbusha tu haitoshi ama kwa sababu agizo tayari lilishatolewa kikubwa ambacho ningeomba ni kwamba ingetolewa time frame, kwamba hizi kamati ziwe zimekwishaundwa ifikapo lini.
Mheshimiwa Naibu Spika, unajua naomba nitoe mfano mdogo, watu wawili wanaweza wakaja kwangu, mmoja akaniambia Ikupa unatakiwa ufanye kazi hii, akaondoka. Mwingine akaniambia Ikupa ifikapo kesho saa tano asubuhi uwe umekwisha kufanya hii kazi. Kwa vyovyote vile mimi nitafanya haraka sana kwa huyu aliyeniambia kesho ifikapo saa tano asubuhi hii kazi iwe imekwishakamilika. Kwa hiyo, niiombe Serikali itoe time frame kwa habari ya huu uundwaji wa hizi kamati ili pia hawa wakuu wa mikoa waweze kujipanga kwa habari ya bajeti na waweze kutoa kipaumbele kwa habari ya uundwaji wa hizi kamati. Muda hautoshi sana kuelezea manufaa ya hizi kamati lakini nafahamu kwamba Waheshimiwa Wabunge mnafahamu na Serikali inafahamu umuhimu wa kamati hizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba niipongeze Serikali kwa kuvikumbusha vyombo vya habari kuhusu kutumia lugha ya alama ama kuajiri wakalimani wa lugha ya alama. Nasema kuwakumbusha kwa sababu mwaka jana ilishatolewa time frame na Waziri mwenye dhamana kwamba ifikapo Machi mwaka huu, 2017, hivi vyombo vya habari viwe tayari vinatumia lugha ya alama ama vimeajiri wakalimani wa lugha ya alama lakini sasa kinachotakiwa ni ufuatiliaji, kwamba ni chombo gani ambacho kinatumia lugha ya alama na ni chombo gani ambacho hakitumii na ni kwa sababu zipi. Kwa hiyo naishauri Serikali, kikubwa sasa hivi si kuvikumbusha tena bali ni kuvifuatilia kwamba ni vipi vinatumia na vipi havitumii kwasababu zipi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee idara ya watu wenye ulemavu. Wakati napitia kwenye randama idara hii haina kifungu na idara hii ina umuhimu mkubwa sana. Tukiongelea vyuo vya watu wenye ulemavu ambavyo sasa hivi ni vyuo vipatavyo vitano vimekwishafungwa na ni vyuo viwili tu ambavyo vinafanya kazi na vyenyewe kwa kusuasua sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Idara hii ina umuhimu sana, itahudumia vyuo vya watu wenye ulemavu, itahudumia hizi sherehe za Kitaifa za watu wenye ulemavu lakini pia itahudumia mafunzo kwa ajili ya watu wenye ulemavu, jambo ambalo sasa kwa kuinyima idara hii kifungu ama kutokuitengea fedha ina maana inakwamisha ufanisi wa haya mambo ambayo nimeyataja.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati naendelea kupitia randama inaonekana kwamba hii idara inahudumiwa kwenye hifadhi za jamii; sasa kwenye hifadhi za jamii sio mambo yote ambayo yamekuwa accommodated, mengi yameachwa kwa sababu bajeti ya pale naona pia sio kubwa
sana. Kwa hiyo niiombe sana Serikali idara hii ni muhimu, ipatiwe kifungu na itengewe fedha ili iweze kufanya kazi yake ipasavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee Baraza la Ushauri la watu wenye ulemavu. Baraza hili ni muhimu, kama ambavyo niliuliza swali mwezi Januari na nikajibiwa kwamba litatengewa fedha. Fedha iliyotengwa ni kidogo, ni kiasi cha Shilingi milioni 4.3 tu ndiyo ambayo imetengwa kwenye hili baraza. Fedha hii haitoshi kwa sababu shughuli za baraza ni kubwa, kwa kikao kimoja inaweza ikatumika shilingi milioni nne mpaka milioni tano, kwa sababu lina wajumbe wapatao 20. Sasa kwa kuitengea shilingi milioni 4.3 hii fedha ni ndogo sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali kwenye hili eneo la baraza fedha iongezeke angalau ifike hata Shilingi milioni 20, katika Shilingi milioni 20 vikao vinavyofanyika ni vinne. Kwa hiyo, kama vinafanyika vikao vinne ina maana hapo tunakuwa na wastani wa angalau Shilingi milioni tano kwa kila kikao, Shilingi milioni 4.3 ni ndogo sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia ikumbukwe kwamba vyanzo vya fedha vya hili baraza mojawapo ni fedha ambazo zinaidhinishwa katika Bunge hili Tukufu na hiki ndicho chanzo pekee cha uhakika vyanzo vingine ni vya wafadhili; wafadhili si chanzo cha uhakika. Nitoe mfano mdogo, mtoto anakuwa na uhakika wa chakula anachopika mama yake nyumbani kwake na si chakula cha kutegemea kwa jirani. Kwa hiyo, niiombe sana Serikali itoe hizi fedha, iongezee hili baraza fedha angalau ifike hata Shilingi milioni 20 ili tuwe na uhakika kwamba hili baraza litafanya kazi kama ambavyo niliahidiwa Januari wakati swali langu linajibiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba niongelee Mfuko wa Watu Wenye Ulemavu. Mfuko huu ni muhimu na hata wakati nachangia mpango mwezi Januari niliongea, kwamba once huu Mfuko utakapopatiwa fedha mambo mengi ya watu wenye ulemavu yatakuwa solved tofauti na
sasa hivi. Unajua tunachoongelea sasa hivi ni kwa sababu hakuna fedha, ni kwa sababu bajeti inayotengwa kwa ajili ya watu wenye ulemavu inakuwa ni ndogo sana ndiyo maana mambo mengi yanakwama.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa, naomba niunge mkono hoja iliyopo Mezani na naomba kuwasilisha.
Ahsante.