Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa. Kwanza nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia sote kufika hapa kwa ajili ya kutimiza wajibu wetu. Vilevile nitumie fursa hii kukupa pole wewe kwa kuondokewa na mmoja kati ya sisi, Mbunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Mheshimiwa Dkt. Macha ambaye alikuwa Mjumbe mwenzangu wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.
Mheshimiwa Spika, nianze kwanza kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu. Nampongeza kwa jambo moja kubwa sana, humbleness. Kwa kipindi cha mwaka mmoja ambao amekuwa Waziri Mkuu wetu ame-portray kuwa kiongozi mtulivu, mwadilifu na msikivu. Simpongezi kwa sababu labda ya unafiki au kuna kitu nataka, this is the naked truth. Ni Waziri Mkuu mpole, msikivu na anayesimamia kile ambacho anakiamini. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tumeshuhudia viongozi wa ngazi mbalimbali na Wabunge wamekuwa wakisema katika levels mbalimbali za wilaya na mikoa viongozi wengi kukosa sifa aliyonayo Mheshimiwa Kassim Majaliwa. Hiki ni kipaji ambacho Mwenyezi Mungu amempa na hatuna budi
kumpongeza kwa kuonesha hilo. Nadhani viongozi wengine katika nchi wana wajibu wa kujifunza jambo hili alilonalo Mheshimiwa Majaliwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, niende kwenye kuchangia. Kwanza niipongeze Ofisi ya Waziri Mkuu, ukiangalia kwenye maelezo ya hotuba yake na Kamati, bajeti ya maendeleo wamepata asilimia 44, ndicho walichokipata. Hii ni taswira inayoonesha kwamba Serikali katika Wizara mbalimbali suala la upelekaji wa fedha limekuwa tatizo. Kwa hiyo, ningeshauri kwenye cabinet kabla ya bajeti ya Serikali Kuu haijaja ingawa katika Kamati tumeona wote, mimi kwenye Kamati niliyopo nimeona utekelezaji wa bajeti ulivyo tatizo hasa fedha za maendeleo.
Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Waziri Mkuu ukiangalia ukurasa wa 16, anapoongelea suala la Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana imetoa mikopo ya 1.5 billion shillings kwa vikundi 297 lakini ameongelea Mamlaka ya Serikali za Mitaa kutoa 4.6 billion lakini tulioshiriki kwenye mchakato huu, mimi nimeenda na Mkoa wangu Serikali za Mitaa kuona ni kiwango gani fedha kutoka Central Government zinavyoathiri upatikanaji wa asilimia tano na asilimia 10.
Mheshimiwa Spika, kwa mfano katika Halmashauri ya Mji wa Nzega, OC iliyokuwa budgeted kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ilikuwa ni shilingi milioni 606, tulichokipokea ni asilimia 27 peke yake. Development budget ilikuwa ni 5.7 billion tulichokipokea ni asilimia 24. Maana yake ni kwamba fedha tulizokusanya katika mapato ya ndani zote zitaenda kusukuma shughuli za uendeshaji wa ofisi, asilimia tano ya akinamama na asilimia tano ya vijana haiwezi kuwa attained. Kwa hiyo, tafsiri ni moja tu, ni lazima tupange realistic budget. Sio vibaya kuwa na uhakika kuliko kujenga matumaini makubwa kwa watu wetu ambayo hayapo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, pale Ofisini kwa Waziri Mkuu na mimi nimpongeze kuanzisha hiki kitengo cha ku- track ahadi za Rais, nampongeza sana. Mheshimiwa Waziri Mkuu ningekuomba uende hatua ya mbele zaidi, ile ofisi yako inayo-track ahadi za Rais kwa mfumo wa kidigitali na utekelezaji wake katika kila Wizara tungeomba angalau kila miezi sita Wabunge tugawiwe, kwa sababu sisi ndio tuliokuwepo kwenye majimbo wakati Rais anatoa hizi ahadi. Zipo ahadi za Ilani na zipo ahadi ambazo Rais alitoa pale pale hadharani. Kwa mfano, katika Jimbo langu Rais aliahidi ujenzi wa daraja la Nhobola na sisi katika Halmashauri tukaamua kutoa fedha imefanyika feasibility study na kila kitu tume-submit Wizara ya Ujenzi, kwa sababu uwezo wa TAMISEMI kujenga haupo.
Mheshimiwa Spika, aAhadi ile tuliahidiwa itatekelezwa mwaka huu mpaka leo hatuoni dhamira pamoja na kukutana na Mawaziri katika corridor. Wakati Rais anakwenda Chato Desemba alifanya mkutano Nzega na kwenye podium akasema kwamba jambo hili linashughulikiwa mwaka huu wa fedha, hakuna, wananchi wanaishi kwa matumaini. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwenye hotuba hii ya Waziri Mkuu amezungumzia suala la kukua kwa uchumi kwa asilimia saba na nimemsikia dada yangu Mheshimiwa Janet Mbene amezungumza suala hili. Economic growth na economic development ni vitu viwili tofauti. Tunapozungumzia growth ya uchumi bila kuzungumzia kubadilika kwa maisha ya watu tutakuwa tunajidanganya kwenye takwimu na tatizo liko wapi? Tatizo la kwanza ndugu zangu nimeangalia alichokipresent Waziri wa Fedha hapa hakuna inclusion, kwenye mpango wetu tunaokuja kuupitisha wa 2017/2018 ni ule ule hauna tofauti na 2016/2017. Hakuna focus kwenye agrosector.
Mheshimiwa Spika, hatuwezi kuondoa matatizo ya watu wetu kama hatuwekezi kwenye kilimo. Ni hatari kweli! Mimi nataka niseme, kama hatutokuwa makini kutatua changamoto ya umaskini wa watu wetu kwa kuangalia sector zinazokua, zinazogusa maisha ya watu, it is just a time bomb, iko siku watu watatafuta haki yao mitaani na hii itahatarisha usalama wa nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, angalia sekta zilizo-contribute asilimia saba kutokana na hotuba ya Waziri Mkuu, madini, usafiri, mawasiliano, financial institution. Madini ni yapi? Ni GGM na Acaccia. Ripoti ya Kamati ya Bomani ambayo iliundwa na Serikali ya Awamu ya Nne mpaka leo utekelezaji wa mapendekezo yake its only 30%. Kamati ya Bomani ilipendekeza mrahaba wa 3% - 15% hiyo ndiyo range. Revenue
sharing plan hatujafanya, matokeo yake tumefanya nini? Ndiyo hii tunafanya zima moto. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tunayo mipango, tuna Sera ya Madini ya nchi, tuna mapendekezo ya ripoti ya Bomani hayajatekelezwa, tunafanya hizi kazi za zima moto. Ningeomba Mheshimiwa Waziri Mkuu niishauri Serikali kwa heshima kabisa, kule kwangu Nzega wanaamini yale makontena yaliyoko pale bandarini ndani yana dhahabu yaani kuna zile gold bar. Tunaomba mrekodi hili tukio la uchunguzi mtuoneshe kwenye TV kilichomo ndani ya zile kontena.
Mheshimiwa Spika, mimi ni mmoja wa watu ambao naamini uwekezaji wa migodi mikubwa haujasaidia nchi yetu. Haujasaidia kabisa na mimi ni muathirika natoka Nzega. Yule Resolute kaondoka na 10 billion shillings ya service levy, nimesema humu, TMA wamefanya, nimeandika barua na kwa taarifa yako Mheshimiwa Spika, mwezi wa Sita anapewa certificate na Serikali ya ku-close mradi na kuondoka. Anaondoka na bilioni kumi ya Watanzania na ya wananchi wa Nzega, it is very painful. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, niishukuru Serikali kwa kugawa maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo, mimi kwangu wameanza kupata. Hata hivyo, naiomba Wizara ya Nishati na Madini, nimpongeze Waziri na Naibu Waziri kwenye hili wamekuwa supportive. Wale mnaowapa leseni wakija
kwenye Halmashauri zetu angalau mhusishe jamii kwa sababu… Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
SPIKA: Mheshimiwa Bashe, muda hauko upande wako.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, ahsante.