Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

Hon. Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia. Awali ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutukutanisha tena katika Bunge hili la bajeti.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa pole kwako wewe kwa kuondokewa na mwenzetu Mheshimiwa Dkt. Elly Macha lakini vile vile nitoe pole kwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Wabunge wote.
Mheshimiwa Spika, kwetu sisi kama Wawakilishi wa Watu Wenye Ulemavu ni pigo kubwa kwa sababu ni miongoni mwa mwenzetu ambaye tulikuwa tukitoa mchango mkubwa katika kuhakikisha kwamba haki za watu wenye ulemavu na kuhakikisha kwamba yale masuala ya watu wenye ulemavu basi yanazungumzwa hapa Bungeni. Nawaomba tu Waheshimiwa Wabunge pamoja na viongozi na Mawaziri kuhakikisha kwamba tunamuenzi Dkt. Elly Macha kwa kuyatimiza yale aliyokuwa akiyapigania humu Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nichukue nafasi hii kwa kuipongeza Serikali pamoja na Mawaziri wote.
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia. Awali ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutukutanisha tena katika Bunge hili la bajeti.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa pole kwako wewe kwa kuondokewa na mwenzetu Mheshimiwa Dkt. Elly Macha lakini vile vile nitoe pole kwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Wabunge wote.
Mheshimiwa Spika, kwetu sisi kama Wawakilishi wa Watu Wenye Ulemavu ni pigo kubwa kwa sababu ni miongoni mwa mwenzetu ambaye tulikuwa tukitoa mchango mkubwa katika kuhakikisha kwamba haki za watu wenye ulemavu na kuhakikisha kwamba yale masuala ya watu wenye ulemavu basi yanazungumzwa hapa Bungeni. Nawaomba tu Waheshimiwa Wabunge pamoja na viongozi na Mawaziri kuhakikisha kwamba tunamuenzi Dkt. Elly Macha kwa kuyatimiza yale aliyokuwa akiyapigania humu Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nichukue nafasi hii kwa kuipongeza Serikali pamoja na Mawaziri wote. kwa kazi kubwa wanayofanya kwa Serikali hii ya Awamu ya Tano. Pia natoa pongezi za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Rais kwa kutambua na kuthamini mchango wa Watu Wenye Ulemavu na kuchukua uamuzi wa kuwapa nafasi katika nyanja mbalimbali na hii inaonesha kwamba kuwa na
ulemavu siyo kulemaa. Hongera sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nijikite tu kwa kutoa ushauri kwa Serikali na hasa nianze kwa suala zima la elimu. Napenda kuishauri Serikali kwamba kwa sababu Serikali imetoa elimu bure kwa elimu ya msingi mpaka sekondari; na hii imekuwa ni faraja kwa sababu miongoni mwa watu ambao
walinyimwa elimu kutokana na mila na tamaduni za jamii za kiafrika na hasa sisi wenyewe. Mfano mzuri tu, hata katika jamii ninayotoka. Kwa
maana hiyo basi, mpango huu wa elimu bure, umesaidia sana kuhakikisha kwamba jamii inawapeleka watoto wenye ulemavu kupata elimu. Katika shule mbalimbali hivi sasa watoto wenye ulemavu wengi wanatambua na wanapata elimu. Kwa hiyo, naipongeza Serikali kwa hilo.
Mheshimiwa Spika, naishauri pia Serikali kuhakikisha kwamba inatimiza wajibu wake kwa kupeleka fedha kwa wakati unaotakiwa ili kuepusha usumbufu na kuhakikisha kwamba hata ile mianya yote ambayo wamekuwa wakitumia baadhi ya watu wasio waadilifu wanaosababisha
fedha hizi kupotea katika njia zisizoeleweka, basi Serikali iwabane na kuweza kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
Mheshimiwa Spika, naungana na Serikali na naipongeza pia kwa kutambua haki ya msingi ya kikatiba kwa Watu Wenye Ulemavu kupata haki ya msingi ya kupata taarifa. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ameeleza dhahiri kwamba Serikali imevitaka vyombo vya habari vihakikishe kwamba vinaajiri Wakalimani ili wenzetu nao waweze kupata taarifa.
Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali na naviomba tu vyombo vya habari kuhakikisha kwamba vinatimiza agizo hili la Serikali kuhakikisha kwamba linaajiri. Namwomba Waziri mwenye dhamana Mheshimiwa George Mwakyembe, ahakikishe kwamba vyombo vya habari vinatimiza wajibu kuajiri wakalimani ili basi viziwi nao waweze kupata taarifa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, napenda pia kuishauri Serikali katika Mfuko wa Watu Wenye Ulemavu; katika bajeti ya mwaka 2016/2017 mfuko wa watu wenye ulemavu haukutengewa fedha.
Mheshimiwa Spika, kama mnavyofahamu, hii ni haki ambayo nchi imeridhia Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu na nchi yetu imeridhia mkataba huo ambao baada ya kuridhia ni kuhakikisha zile haki za watu wenye ulemavu zinatimizwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mfuko huu katika bajeti iliyopita inayoishia katika Bunge hili haukuweza kutengewa fedha, kwa hiyo, naishauri tu Serikali kuhakikisha kwamba mwaka huu fedha hizo zinafanya kazi, kwa sababu mfuko huu utakapotengewa fedha ni kwamba Baraza la Watu
wenye Ulemavu litaweza kufanya kazi na litakuwa ni msaada mkubwa katika kuishauri Serikali katika nyanja mbalimbali na hasa masuala mbalimbali yanayowahusu Watu Wenye Ulemavu.
Mheshimiwa Spika, kwa sababu Serikali ya Awamu ya Tano ina nia ya dhati kabisa katika kuhakikisha kwamba inashughulika na masuala ya watu wenye ulemavu, kwa hiyo, nisisitize tu kwa kusema kwamba, hili ni jambo jema, lakini tuhakikishe kwamba linaendana na fedha ili basi Baraza hili liweze kufanya kazi na kushughulikia changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa huduma kwa watu wenye ulemavu na katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu imeelezea ni jinsi gani basi ambavyo inatambua na itaendelea kutoa huduma kwa watu wenye ulemavu. Pamoja na kauli hii, kumekuwa na
changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikiwakabili watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Spika, kwa mfano, Serikali imekuwa na utaratibu mzuri tu kwa watoto wasioona, zipo shule maalum ambazo zimetengwa na shule hizo wamekuwa wakienda hawa watoto kupata elimu na wamekuwa wakilipiwa gharama mbalimbali na hasa nauli kwa sababu jamii
haitambui mchango wa watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiwapa nauli na kuwapeleka katika shule zilizotengwa. Mfano Shule ya Uhuru Mchanganyiko, lakini kuna shule nyingine ipo Iringa.
Mheshimiwa Spika, tatizo lililopo hivi sasa wale watoto wanapokwenda na inapofika wakati wa likizo hawawezi kwenda nyumbani na matokeo yake wanabaki mwaka mzima huko huko. Kwa sababu wazazi wengi hawatambui hilo na tayari walikuwa wamezoeshwa hivyo, kwa hiyo, wale
watoto wanakuwa hawana tena nafasi ya kurudi majumbani.
Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali ije na majibu kwamba je, ni kweli wao ndio wametoa agizo hilo kwamba hakuna fedha kwa ajili ya watoto hawa au ni baadhi ya Walimu wa hizi shule ambao wamekuwa wakijichukulia madaraka wao wenyewe na kuamua maamuzi kwamba watoto hawa wasirudi nyumbani?
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nitamwomba sana Mheshimiwa Waziri wakati wa kuhitimisha bajeti hii basi aweze kutoa hizo taarifa ili tuweze kujua ni jinsi gani tunaweza kuwasaidia watoto hawa ili na wao pia waweze kupata elimu; na kama mnavyofahamu elimu ndio ufunguo wa
maisha.
Mheshimiwa Spika, unapomsaidia mtoto mwenye ulemavu akapata elimu, umemwokoa na mambo mengi. Mara nyingi nimekuwa nikitoa mfano kwamba sisi tusingesoma hizi nafasi hapa tusingeweza kupata. Kwa hiyo, ili tuweze kujikomboa sisi wenyewe elimu ndiyo msingi na
elimu ndiyo silaha yetu ili tuweze kujisaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hilo, nisemee suala la Mahakama. Katika suala la Mahakama tuhakikishe tu kwamba zile kesi ambazo walikuwa wamehukumiwa wale watu au kesi ambazo zinaendelea katika Mahakama mbalimbali nipate tu takwimu ni wangapi wamehukumiwa? Wangapi ambao bado kesi zao zinaendelea? Vile vile tujue kama kumekuwa na taarifa nyingine za mauaji ya watu
wenye ulemavu wa ngozi.
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.