Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Hoja ya kwanza ambayo nitaanza nayo ni ya viroba kwa sababu nilielekezwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu niongoze kikosi kazi cha Serikali cha kushughulikia suala hili ambacho kilihusisha Wizara na taasisi mbalimbali za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka hivi tunavyoongea suala hili linaelekea ukingoni na pengine baada ya miezi mitatu viroba vitapigwa marufuku kabisa katika nchi hii na wala sio suala la kusema viroba vitaruhusiwa kuuzwa labda kwenye maeneo maalum kama bar ama kwenye vioski na vitu kama hivyo na vitoke kwenye maduka ya kawaida, tunaelekea kwenda ku-ban kabisa (total ban) ya matumizi ya viroba katika nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia suala la usagaji na mambo ya ushoga, nalo tumelishughulikia sana ndani ya Serikali na mimi mwenyewe nimeongoza kikosi kazi cha kufanya tathmini ya suala hili. Hivi tunavyoongea kuna taasisi mbalimbali ambazo zilikuwa zinajihusisha na uhamasishaji wa vitendo vya ushoga zipo katika uchunguzi na nyingine tumezifutia usajili na hazifanyi kazi katika nchi yetu. Tutaendelea kuchukua hatua dhidi ya watu wote wale ambao watapingana na tamaduni zetu ambazo zinalindwa na sheria ambayo tuliipitisha hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hapa kuna Wabunge wameniletea taarifa za shoga mmoja maarufu kwa jina la James Delicious ambaye anajiuza kwenye mitandao. Namuagiza Katibu Mkuu afuatilie taarifa hizi ili shoga huyu aweze kuchukuliwa hatua haraka iwezekanavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu kwamba watumiaji wa dawa za kulevya huku tunawakamata lakini kwa upande mwingine tunawapa tiba. Hii inajulikana kama public health approach kwamba hatuwezi kuwakamata watu wanaotumia na tukawachukulia hatua badala yake tuna jukumu la kibinadamu la kuwahudumia kama wameamua kufuata huduma kwenye vituo vya kutolea huduma. Kwa hiyo, suala la udhibiti lina sheria na taratibu zake, lakini pia suala la kuhudumia waliothirika lina taratibu zake kwa mujibu wa sheria na kanuni mbalimbali za afya za kitaifa na za kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la watumishi kwenye sekta ya afya, ni kweli tunakiri upungufu kwa sababu katika miaka miwili iliyopita, kwa tathmini tuliyoifanya mwaka 2016 tulipaswa kuwa na watumishi wapatao 179,509 lakini tunao 90,000 tu sawa na 51%. Kwa hiyo, tuna upungufu mkubwa, tunaufahamu na tunaendelea kuushughulikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine lililojitokeza ni suala la Ocean Road Cancer Institute kuwa na vifaa vilivyochakaa. Suala hili tunalifahamu na tayari Serikali imeweka kipaumbele cha kipekee kwenye taasisi hii inayotibu magonjwa ya saratani na hivi ninavyoongea hapa, bajeti ya dawa kwenye kituo hiki imepanda kutoka shilingi milioni 700 mwaka uliopita mpaka shilingi bilioni saba mwaka wa fedha ambao unaendelea. Mpaka kufikia Disemba tayari Ocean Road walikuwa wamepatiwa bajeti ya shilingi bilioni tatu na sasa hivi upungufu wa dawa kwa kweli umepungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, tumeongeza idadi ya vitanda kutoka 40 mpaka 100 kwa wagonjwa wanaopokea tiba ya saratani kwa njia ya dawa na hivyo msongamano umepungua sana. Kwa sasa Serikali ina mikakati ya kuanzisha huduma za tiba ya saratani kwenye vituo vingine mbalimbali kwenye kanda nne za nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, KCMC kufikia Disemba walianzisha huduma ya tiba kwa dawa (chemotherapy), lakini Bugando mwezi Machi wataanza kutoa tiba ya mionzi kwa mara ya kwanza toka tupate uhuru ya ugonjwa wa saratani ambayo ilikuwa haijawahi kutolewa hata siku moja nje ya Kituo cha Ocean Road.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi Hospitali yetu ya Kanda ya Rufaa ya Nyanda za Juu Kusini, pale Mbeya na yenyewe kufikia Julai itaanza kutoka huduma za tiba ya sarani kwa njia ya mionzi pale pale ili ku-off load mzigo wa wagonjwa ambao wangelazimika kuja mpaka Ocean Road kwa ajili ya kupata tiba hiyo. Sasa watapata kule kule Nyanda za Juu Kusini na tutaendelea kushusha huduma hizi karibu zaidi na wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kulikuwa kuna hoja ya makazi ya wazee kwamba yamechakaa. Hili tunalifahamu na tulishalichukulia hatua. Hivi sasa tunavyoongea hapa vituo kumi vya kuhudumia wazee vinafanyiwa ukarabati kwenye maeneo ya majiko na vyoo, lakini pia tutavipelekea bajaji kwa ajili ya kuwasaidia wazee waweze kupata huduma za kupelekwa hospitali na maeneo mengine kirahisi zaidi.