Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza, niipongeze sana Kamati kwa ushauri mkubwa ambao imetupatia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la VETA, napenda kusema kwamba tunakubaliana kwamba lazima tuangalie course zake zinazoendelea kutolewa ili kuendana na hali halisi ya uhitaji wa soko na ujuzi tunaohitaji katika uchumi wa viwanda na biashara. Mfano tu kwa siku za nyuma katika baadhi ya maeneo watu binafsi walikuwa wanaruhusiwa kufanya kazi za umeme wa majumbani tu lakini sasa hivi wanaruhusiwa kufanya kazi hata za kuweka vituo vya umeme, jenereta na hata ujenzi wa laini. Kwa hiyo, na sisi tutarekebisha mitaala yetu kadri tunavyoenda ili kuweza kufikia hali inayoendana na soko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kuhusiana na UDOM. Serikali haikuwaondoa wanafunzi wa UDOM ili tuweze kuhamia pale. Nachotaka kusema tu ni kwamba Serikali itaendelea wakati wote kuboresha mambo yote ambayo inaona kwamba yana tija kwa nchi. Kimsingi Chuo cha UDOM tuliweka nia njema ya kupeleka wale wanafunzi pale ili tupate hawa wanafunzi kwa ajili ya masomo ya sayansi na hisabati lakini likajitokeza tatizo kubwa la walimu jambo ambalo liliashiria hata kuleta migomo ya walimu yaani wahadhiri. Nafahamu kwamba hata Mheshimiwa aliyetoa hoja aliwahi kunielezea kuna tatizo gani kuhusiana na hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipotafakari tukaona kwamba wanafunzi hawa wanaweza wakapelekwa kwenye vyuo ambavyo tayari kuna walimu, ndivyo tulivyofanya, vilevile katika vyuo hivyo tulikuja kugundua kwamba hata ada yao ni pungufu kuliko hata ile ambayo ilikuwa inalipwa UDOM kwa kozi ileile. Kwa misingi hiyo unakuta kwamba ada iliyokuwa inalipwa UDOM inatosha kulipia watu wanne. Kwa hiyo, imekuwa ni tija kuwapeleka huko na wanafunzi wenyewe wanakiri kuwepo kule wanapata ufundishwaji unaostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niseme tu kwamba kwa Serikali kuhamia na kutumia majengo yale kwa sasa ni jambo ambalo lina tija, kwa sababu majengo yale yalijengwa kwa mkopo unaolipwa na Serikali na Serikali haioni tija kupanga majengo mengine wakati kuna majengo ambayo kwa sasa hayatumiki yakingojea kuendelea kuongeza walimu wa kutosheleza majengo yote.
Kwa hiyo, niseme tu kwamba pale Serikali ipo kwa muda na tunaendelea kupokea ushauri wa Kamati ya Bunge kwamba baada ya hapo tutaendelea na ujenzi katika maeneo yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie kidogo suala hili la ufaulu. Nitoe mfano wa maisha ya kawaida. Unaweza ukawa kila siku unamwona mume au mke wako siyo mzuri ukafikiria mume au mke wa jirani mzuri kwa sababu anakula nyama kila siku, ukafikiria wa kwako sivyo. Tumezisema sana na kuzisimanga shule hizi ambazo ni za kwetu za kata kwamba labda hazifanyi vizuri. Nataka tu niwaeleze ukweli na hili nalisema kwa ajili ya kusaidia kuiona Serikali imefanya nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda mnielewe naposema hivi simaanishi kwamba shule hizo zinafanya vizuri sana, hapana, nakubaliana kabisa kuendelea kuboresha. Nachojaribu kusema ni kwamba ukienda ndani katika matokeo ya hizi shule, kwa mfano shule ya Kibaha utakuta watoto waliofaulu division one ni 72, division two ni 22, division three ni nne na division four mmoja.
Kutokana na hiyo division four na one wamewavuta kwenye ufaulu wao kiasi cha kuwaweka ni watu wa 16, lakini ukienda Feza hiyo ambayo tunasema imekuwa ya kwanza yenyewe ina wanafunzi 65 na division one ni 59 na division two ni sita. Kwa hiyo, ukiangalia kwa idadi ya watu utakuta kwamba shule imefanya kazi kubwa. Hali kadhalika ukienda katika shule nyingine, kama shule ya Kilimanjaro utaona hivyo hivyo, inaonyesha hapa division one ni 44, division two ni 44, na division three ni 31 lakini kuna 68 ambao ndio wanawavuta wenzao. Kwa hiyo, si kwamba shule za Serikali hazichangii zina mchango mkuwa sana.
Toka shule za kata zimeanzishwa zimechangia jumla ya watu waliopata division one mpaka three 180,542, hayo ni mafanikio makubwa sana kwa Serikali yetu.