Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru kwa kunipa nafasi na mimi nichangie kwa hizi dakika tano zilizosalia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na wale wote walio katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya na michango iliyotolewa Bungeni nawashukuru sana, niendelee katika vipengele vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la miundombinu ni tatizo na wengi wamezungumzia katika vyuo vikuu ambako pia kuna changamoto kubwa lakini pia tukiangalia katika shule za msingi na sekondari changamoto bado ni kubwa sana, mfano mabinti wengi hasa vijijini kutokana na uhaba wa mabweni hawafiki mbali zaidi. Pia kama tunavyofahamu mabinti wanakabiliwa na changamoto mbalimbali mfano tu binti anapokuwa katika siku zake za hedhi nayo ni changamoto kubwa hata Kamati imeeleza basi Wizara iangalie ni jinsi gani inaweza kusaidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwa wototo wenye ulemavu ambao ni changamoto kubwa sana. Naishukuru Serikali kwa suala zima la elimu bure kwa wote ambalo limesaidia kwa kiasi kikubwa wazazi wenye watoto wenye ulemavu kuwaandikisha watoto hawa shule. Siku za nyuma mzazi kama ana watoto wawili, watatu lakini ana mtoto mwenye ulemavu ni afadhali awapeleke hawa wengine, mwenye ulemavu anabaki nyuma. Kwa utafiti mdogo ambao binafsi nimeufanya watoto wenye ulemavu wengi hivi sasa wameandikishwa shule lakini changamoto ni nyingi katika shule zetu mbalimbali. Kwa hiyo, niiombe tu Wizara ihakikishe kwamba watoto wanaweza na wao kupata haki yao ya msingi ya kupata elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliuliza hata juzi katika vyuo vyetu vikuu changamoto bado ni kubwa kwa wale wanafunzi wenye ulemavu wanaopata bahati ya kwenda vyuo vikuu. Niiombe tu Serikali kupitia Wizara husika hasa katika vyuo vikuu na mfano mojawapo ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambacho miuondombinu ni tatizo. Kwa wanafunzi wanaopata bahati kwenda katika vyuo vikuu na hasa chuo hiki cha Mlimani ni tatizo kubwa kutoka darasa moja kwenda darasa lingine. Ukiangalia mazingira yenyewe katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hawawezi kupata elimu ipasavyo na wanafunzi hawa wengi wao hata matokeo yanapokuja siyo mazuri sana. Wanaopata matokeo mazuri ni bahati.
Kwa hiyo, kutokana na changamoto hii, naiomba Serikali kuangalia ni jinsi gani itaboresha miundombinu ili wanafunzi wenye ulemavu waweze kusoma pasipo changamoto yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niangalie pia katika Shirika la Utangazaji Tanzania na ni-declare tu interest kwamba mimi mwenyewe nimetoka huko. Nasikitika sana kwa Serikali kwa jinsi ambavyo kwa muda mrefu imekuwa ikisuasua kupeleka fedha na hata katika ripoti hii ukiangalia ni kwamba kila mwaka bajeti hiyo inapungua. Mimi nina imani sana na viongozi wetu walioko katika Wizara hii lakini watawezaje kutekeleza majukumu yao endapo bajeti hizi haziwezi kufika? Mheshimiwa Rais amemteua Ayub Rioba kuwa Mkurugenzi nina imani naye, lakini kama hakuna bajeti miundombinu ni chakavu, mitambo imechoka na iliyopo imezeeka ya tangu mwaka 1999...
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba tu Serikali kuhakiksha kwamba bajeti hii inaifikisha katika Wizara hii ili waweze kutoa kwa TBC.