Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nizungumzie suala la fedha kidogo ambazo zimepelekwa kwa ajili ya maendeleo ya viwanda. Nisisitize tu kwamba utoaji wa fedha unategemea sana upatikanaji wa mapato. Kwa kifupi revenue effort yetu kwakweli bado haitoshi kubeba mzigo mkubwa wa mahitaji yetu kitaifa. Tumefanya vizuri, nilieleza upande wa domestic revenue lakini tumepata changamoto upande wa misaada na mikopo katika nusu ya kwanza lakini tunaendelea kulifanyia kazi na prospects, matumaini yetu ni makubwa katika nusu ya pili ya mwaka iliyobaki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili nisisitize kuwa fedha hizi zilizotolewa si kwa ajili ya kujenga viwanda. Fedha hizi ni kuiwezesha Wizara kufanya facilitation, ni kuiwezesha Wizara kuweza kuielekeza sekta binafsi wapi wawekeze. Kwa hiyo, hizi sio fedha kwa ajili hiyo, msimtegemee kwa kweli Waziri kujenga viwanda na Mheshimiwa Ridhiwani amelieleza vizuri lakini pia Mheshimiwa Mary Nagu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa kweli miezi saba ni kipindi kifupi sana kuweza kufanya evaluation kwamba Serikali imepiga hatua kujenga viwanda. Utaratibu wa kujenga viwanda hii ni long term na tujielekeze zaidi kwamba sekta binafsi katika kipindi hiki imejenga viwanda gani na Serikali ime-facilitate kiasi gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba kwa kweli Serikali imejitahidi kufanya vitu ambavyo ni msingi wa viwanda, kwa hiyo, mnapo evaluate kwamba Serikali imefanya nini kujenga viwanda muangalie effort ya Serikali upande wa umeme, upande wa miundombinu mingine ya maji na usafirishaji, lakini pia jitihada mbalimbali ambazo zimefanyika katika kuhamasisha uwekezaji wa ndani ya nchi. Ningeweza kulieleza kwa kirefu lakini niishie hapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusu madeni ya mifuko. Niseme tu kwamba ilikuwa muhimu kwanza Serikali ifanye uhakiki wa yale madai ya kwanza yaliyowasilishwa; na kwa kweli hali ilikuwa si nzuri hata kidogo. Yale madai yaliyowasilishwa tuligundua kwamba kulikuwa na sehemu kubwa ambayo si madai halali na hasa kwa upande wa miradi ya ujenzi ambayo ilitumia fedha hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaangalia sasa upya ule mkakati wetu wa kulipa yale madeni, ikiwa ni pamoja na issuance ya ile special cash bond ya shilingi bilioni 290 na tunatarajia kwamba hizi taratibu zitakamilika hivi karibuni ikiwa ni pamoja na jitihada za kupata fedha pia mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia kutusaidia kulipa madeni hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kukosekana Bodi ya Wakurugenzi wa Mashirika na hasa ilisemwa TANAPA, naomba niliambie Bunge lako Tukufu kwamba Serikali tumefanya jitihada na tumeshakamilisha uteuzi wa bodi za taasisi mbalimbali ikiwemo hii ya TANAPA na Bodi hii ya TANAPA inaongozwa na Bwana George Waitara. Kwa hiyo, tumefanya jitihada mbalimbali katika kukamilisha shughuli hizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niseme lingine pia ni kuhusu bajeti ndogo ya ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, ni kweli fedha hizi ni kidogo, na niseme tu kwamba si ofisi peke yake ambayo haijapatiwa fedha, tatizo kama nilivyosema ni sungura mdogo. Sasa hivi tunakamilisha mapitio ya utekelezaji ya nusu mwaka na kwa hakika tutalitazama hili kwa kuzingatia unyeti wa sekta ya mazingira na athari ambazo zinaonekana wazi. Lakini ukweli unabaki pale pale kwamba kwa kweli mahitaji yetu ni makubwa, tunahitaji sana kujiwekea vipaumbele vya dhati ndani ya sekta na kwa Taifa letu kwa ujumla ili kuweza kuelekeza…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Vizuri sana Mheshimiwa Waziri.