Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia maneno mawili, matatu hususani kuhusu viwanda na mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote mimi nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayoifanya, lakini nitoe masikitiko yangu makubwa, kama leo Baba wa Taifa ingekuwa kuna jambo la kusema anaweza akasimama akauliza, angeuliza habari ya Tabora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tabora tuna mateso sana, tulikuwa na viwanda vifuatavyo kwa sababu ni dakika tano lakini nilikuwa nimejipanga kwa dakika kumi ningeeleza nadhani leo Mheshimiwa Waziri yangemuingia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Tuna Kiwanda cha Nyuzi na Mheshimiwa Riziki amesema, kiwanda hiki kimehujumiwa na wawekezaji. Wamechukua kila kitu hata kama tunakwenda kwa science na teknolojia wameondoa vifaa vyote na wametapeli, mimi ninasema kwa lugha nyepesi, wametapeli. Tangu wamechukua hawajafanya chochote; kwa hiyo hata tukisema zao la pamba liweze kuimarishwa hakuna, tulikuwa tunatengeneza nyuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti lakini tuna Kiwanda cha kusikitisha sana cha Manonga, Mheshimiwa Waziri anajua kipo Igunga. Kiwanda hiki alikuwa amechukua Rajan. Mimi mwaka 2006 nikiwa Mbunge niliwahi kuuliza swali, lakini huyu mwekezaji Rajan amefariki, wamechukua watoto wake, bado kuna usumbufu mkubwa tangu mwaka 1999 kiwanda kile kimefungwa. Ni uchungu mkubwa sana wa unyanyasaji wa Mkoa wa Tabora. Lakini pamoja na hayo, Mheshimiwa Waziri anajua, tulimuomba awakutanishe Rajan pamoja na Igembe Nsabu, hajafanya hivyo na alitoa ahadi ya kwenda kuongea nao, nina uchungu sana, inasikitisha na inakatisha tamaa.
Mheshimiwa mwenyekiti, si hilo tu, Mheshimiwa Waziri alisema katika Bunge lako hili wakati tunauliza swali na alisema wawekezaji wa Kichina wameishia airport, sasa hivi mpaka leo bado wameishia airport? Inasikitisha, leo nipate majibu kama kweli wawekezaji hawa wapo au hawapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vigezo vya kutafuta wawekezaji Tabora inayo, jinsi ya kuiuza Tabora ipo. Tuna masuala ya tumbaku, tuna masuala ya urinaji wa asali. Hivi asali yote inayotoka nchi nzima hii inatoka Tabora bado hakuna uwezekano wa kuweka kweli? Mheshimiwa Waziri, namheshimu sana naomba aangalie hilo.
Mheshimiwa Mweyekiti, lakini nizungumzie habari ya mazingira. Tabora inalima tumbaku, lakini hawa wanunuzi hawana mpango wa kuhakikisha mazingira endelevu yapo katika Mkoa wa Tabora. Kwa nini nasema hivyo? Wanabeba mbegu za miche, wanatupa kuwapa…….
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante.