Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nimshukuru Mwenyezi Mungu kunijaalia kupata nafasi na mimi kuchangia kidogo na nikushukuru na wewe kwa kunipa nafasi hii na shukrani kwa pekee zizidi kwako na nikuhakikishie tu kwamba uwepo wako katika kiti hicho unatupa raha ndani ya roho zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nataka nizungumzie nikiwa nimejieleza wazi kwamba ni Mjumbe wa Kamati hii ya Viwanda na Biashara na nimpongeze kwa dhati Mwenyekiti wetu. Kati ya Wenyeviti makini wa Kamati hizi za Bunge, Mheshimiwa Dalaly Peter Kafumu naweza kusema ni nambari moja.
Sasa katika Kamati zetu siku moja, alikuja mchumi fulani akatuambia kwamba wawekezaji ni kama ndege, kule wanapokuwa wanaruka angani wanaangalia ni nchi gani inafaa kuwekeza ndipo wanaleta uwekezaji wao. Na kati ya vigezo muhimu sana vinavyowavuta wawekezaji na vivutio muhimu sana, kimojawapo ni amani na usalama katika nchi. Wawekezaji wanaangalia mazingira ya usalama ndani ya nchi, hayo yanawafanya wawe na umuhimu wa kukaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwenendo tunaokwenda nao sasa hauashirii kuwakaribisha wawekezaji katika nchi yetu. Juzi tu hapa wakati nauliza swali nilimshukuru Mwenyezi Mungu sana kwa kuijaalia nchi yetu kuwa ni miongoni mwa nchi ambazo haziko katika janga, tishio la ugaidi, hili ni jambo la kushukuru sana na tumuombe Mungu azidishe hilo. Lakini jambo la kusikitisha, Mheshimiwa Waziri, ninaemuheshimu sana alikuja akalipinga hilo na akaona kwake yeye ni bora kusema kama nchi yetu ni miongoni mwa nchi zilizo katika tishio hilo, ni kitu cha ajabu sana. Mimi namheshimu sana Mheshimiwa Mwakyembe, lakini ningeweza nikadhani labda sijui kuna kitu kimemvuruga au vipi lakini tuyaache hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hilo dogo, leo hii tunashuhudia vitu vya aibu ambavyo vinafanyika ndani ya nchi. Leo hii mtu mmoja anayejipa madaraka ambae aliwahi kujiita Mungu wa Dar es Salaam anafikia hadi ya kutaja majina ya wawekezaji na wafanyabiashara wakubwa kwamba hao ni drug dealers wakubwa sana, kitu ambacho wale wawekezaji tayari wanatafakari upya na kuendelea kuwekeza kwao, je, hawa walioko nje watajifikiriaje kuja kuwekeza katika nchi yetu? Upande mmoja tunahimiza wawekezaji waje kuweka viwanda, upande wa pili tunawa-harass wawekezaji juu ya uwekezaji wao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii ina mfumo kamili wa ulinzi wala sidhani kama umetetereka. Kuna Jeshi la Polisi, kuna Waziri wa Mambo ya Ndani makini sana tunayemuamini, mchapa kazi, kuna vyombo vya ulinzi wa usalama makini sana, kuna Usalama wa Taifa tunaamini ni makini sana, kuna Jeshi la Ulinzi ni makini sana. Leo vyombo vyote hivi vimeonekana havina maana, father god wa Dar es Salaam aliyejiita Mungu wa Dar es Salaam ndiye amejipa jukumu la kusema kila kitu katika nchi hii? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mungu wa Dar es Salaam leo anaweza kumtaja yoyote na isiwe lolote siku ya pili anatoa amri aje central police, ni nani huyu katika nchi hii?
Waheshimiwa Wabunge, vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vilipopewa jukumu la kusimamia mambo haya muhimu ya ulinzi na usalama, dawa za kulevya na everything vimelala wapi? Vinamuachia Makonda aliyejibatiza kujiita Mungu leo anafanya kila kitu, ni nini, what for, tunakwenda wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi leo nataka niliseme hili kwa sababu azma ya kuwekeza kwenye viwanda haiwezi kwenda kwa matamshi ya ajabu ajabu na maamuzi yanayotolewa na mtu mmoja kwa sababu yeye kauli yake inaonekana inasikilizwa sana na Mheshimiwa Mtukufu Rais, haiwezekani. Mimi nadhani sasa kila mmoja atajua wajibu wake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa la mwisho mimi nataka kumwambia ndugu yangu Waziri, Mheshimiwa Waziri nia yako nzuri ya kuimarisha viwanda na mimi nakubaliana na wewe lakini Mheshimiwa Waziri kila mchezo una sheria zake. Kwenye riadha ile kuna mbio za vijiti. Huwezi kukimbia tu ukafika…..
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante,