Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuzingatia kuwa ninazo dakika tano tu nitaongelea hoja mbili. Naomba nibainishe kwamba mimi ni Mjumbe wa Kamati, sote kwa pamoja tuna nia ya kujenga Tanzania ya viwanda; lakini kwa masikitiko makubwa baadhi ya wawekezaji tunaowakabidhi viwanda hivi ili watusaidie kuviboresha kwa kuleta teknolojia za kisasa, wao badala ya kufikiria kujenga Tanzania ya viwanda wanafikiria kujenga Tanzania ya ma-godown. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mzuri ni kiwanda chetu cha nguo cha Urafiki. Tulipotemebelea sehemu ile tulishangazwa na tulishtuka kuona Mkurugenzi Mkuu hajui mission kwa nini wapo pale na hajui vision kwa nini wapo pale, jambo hili lilitusikitisha sana. Lakini baadaye tukabaini kwamba wakati fulani zilitolewa fedha kwa ajili ya kununua mitambo, fedha zilitumia lakini hakuna mtambo hata mmoja ulioletwa, kwa hiyo ulinunuliwa mtambo hewa. Wakati Serikali inahangaika na watumishi hewa wakati umefika pia kubaini mitambo hewa inayonunuliwa, badala ya kuendesha kiwanda, inanunuliwa mitambo hewa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia tulibaini kuna mpango wa makusudi wa kuhakikisha spare ambazo zinatakiwa kutumika kwenye kile kiwanda hazinunuliwi na wala haziagizwi, mashine inapoharibika inabidi sasa ing‟olewe kwa sababu hakuna spare, huo ni mkakati wa kubadilisha kile kiwanda kuwa godown. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tukabaini kwamba pamoja na kung‟oa ile mitambo pale kuna menejimenti mbili; kuna menejimenti inayoongozwa na wazawa na kuna menejimenti inayoongozwa na wawekezaji. Wawekezaji wanajua ya kwao na wazawa wenzetu wanajua ya kwao. Kwa hiyo, ni menejimenti mbili katika kiwanda kimoja, matokeo yake hakuna kinachoendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ya pili ambayo ningependa niimalizie na nyingine niziache, tumeona tatizo la kutotenga fedha za kulipa fidia, kaka yangu Mheshimiwa Mwijage anajitahidi kuhangaika lakini kwa mfano pale Omkajunguti tunataka kuweka Export Processing Zone, zinatakiwa fedha za kulipa fidia, lakini hadi sasa tumeendelea kuzungumza tu hakuna fedha iliyotolewa. Labda tu nimshauri waziri muhusika kwa kuwa alishaniaidi kulipa fidia hizo, alisema ifikapo mwezi wa kumi atakuwa amelipa na sasa hajalipa, ikifika wakati wa bajeti tusigombane, nitafuata taratibu za Kibunge zinazotakiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.