Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nitumie fursa hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu, kwa kutupatia fursa sote kukutana katika kikao hiki, lakini nitumie nafasi hii vile vile kumpongeza na kumtakia kila la kheri Rais wa Awamu ya Tano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tu niseme ujumbe mmoja kuna popular speech aliwahi kuitoa Baba wa Taifa Mkoani Tabora, ambayo alikuwa anazungumzia historia na hadithi ya vijana wanaokwenda kuchumbia kwa binti mzuri lakini wakawa wanazomewa zomewa ukigeuka unageuka jiwe. Kwa hiyo, nimwombe tu kelele nyingi zinaweza zikawepo, asikubali kugeuka jiwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa masikitiko, masikitiko yangu ni kwamba, ni aidha kuna disconnection kati ya vision na mwelekeo wa Rais na walio chini wanaoandaa Mipango mikakati kufikia vision hiyo. Jambo la kwanza ambalo naona wengi wetu tunaimba viwanda, viwanda, tunasahau kwamba viwanda ni matokeo ya efficiency ya sekta zingine, ndiyo tutapata viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nature ya nchi yetu hakuna viwanda kama sekta ya kilimo haitopewa kipaumbele kinachostahili, hakuna viwanda kama sekta ya usafirishaji haitopewa kipaumbele kinachostahili na nianze kuwaambia Wabunge wenzangu tunaosema reli ya kati tunapongeza, hakuna reli ya kati. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma kitabu hiki nendeni ukurasa wa kumi na saba mkasome, naomba ninukuu construction of new Central Railway Lane to standard gauge, ukienda chini sehemu inayosema this project is facing number of challenges as follows. Kipengele namba tatu, the choice of route that is Dar es Salam, Tabora, Kigoma with branches to Tabora Mwanza, and Kaliua - Mpanda, Dar es Salaam – Isaka – Kigali – Keza - Msongati has not been decided, and this is the railway we want.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatutaki railway ya project ya ADB, inayotoka Dar es Salaam kwenda Isaka, kwenda Keza, this does not help this country na niwaombe wenzangu wa Kanda ya Ziwa na Mikoa inayopita reli, hakuna reli yetu, haipo! Hilo ni jambo la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, nimesoma Mpango wa Serikali, Mpango wa Mwaka Mmoja unatokana na Mpango wa Miaka Mitano. Serikali inataka kufufua General Tyre, mmeshafanya study kujua kwa nini General Tyre ilikufa, you are going to allocate two billion shillings kwa ajili ya General Tyre.
Swali la kujiuliza hii General Tyre ni wangapi wamewekeza, nendeni kwenye rekodi NSSF iliwekeza nine billion shillings imeshindikana kufufuliwa kile kiwanda, leo mnapeleka fedha za walipa kodi kwenda kuwekeza kwenye dead project lakini study zipo, wamekuja wawekezaji na Waziri Mwijage anajua, wameomba wawekeze sixty billion shillings kwa ajili ya kufanya investment kwenye kile kiwanda, leo mnataka kuchukua fedha za umma kuweka hapo, this is wrong thinking. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema tunawekeza ATC, hebu jamani tufanye study airline industry, Kenya Airways ambayo partner wake ni KLM mwaka jana wame-register two million U.S dollar loss. South African Airline kila mwaka inapoteza one million U.S dollar, sasa hivi wanataka kuunganisha Airlines tatu ku-streamline operation zao, sisi ATC toka Mwalimu Nyerere, kaja Mzee Mwinyi, kaja Mzee Mkapa, kaja Mzee Kikwete tumeshindwa ku- revive!
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba Serikali fedha za umma kupeleka kununua ndege is wrong direction, lazima tufanye business sense decision siyo kila maamuzi jamani ya kisiasa. Hizi ni fedha za walipa kodi, fedha hizi tuzipeleke kwenye huduma za jamii, fedha hizi tuzipeleke kwenda ku-revive Textile Industry, Mwigulu hayupo hapa, yupo nimemuona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Mpango wa Mwaka Mmoja, ukisoma Mpango wa Miaka Mitano, hapa wanazungumzia C to C na hakuna strategy, wanaelezea tu cotton to clothes, hawasemi wanafanya nini, there is no investment kwenye cotton. Niwaambieni watu wa maeneo tunayozalisha pamba hakuna investment kwenye Mpango wa Miaka Mitano, hakuna investment kwenye Mpango wa Mwaka Mmoja. Hatuwezi ku-revive uchumi wa nchi hii kwa kwenda kuwekeza kwenye mpunga, Serikali inatenga fedha kwa ajili ya mpunga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namshauri Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Mwigulu, nimekutana nae private as my brother and friend, nchi hii tunazalisha mazao mengi fanya strategic decision. Mazao mengine waachie District Commissioners mahindi, mchele, mbaazi, mananasi tuwaachie kwenye Wilaya. Chukua mazao ya msingi, chukua cotton, chukua kahawa, chukua korosho, chukua katani, chukua tumbaku, mazao haya yata-turn around na kumsaidia Waziri wa Viwanda na Biashara, Mheshimiwa Mwijage kuweza kufanikisha wazo la kuwa na viwanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunajadili ufugaji, na-declare interest mimi ni mfugaji, tunajadili kama ufugaji ni jambo la ajabu, mkulima leo akilima heka mbili mwaka kesho akalima heka tatu tunasema growth, mfugaji akiwa na ng‟ombe tatu zikafika saba anaharibu mazingira!
Tanzania ni nchi ya pili Afrika kwa kuwa na mifugo mingi baada ya Ethiopia. Kwa mwaka 2015 Ethiopia kwa tannery industry imewaingizia five hundred million US dollar, leo Kenya wanajenga kijiji cha viwanda vya ngozi, raw material yao sehemu kubwa wanachukua Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, what is the plan? Ukisoma kitabu cha Miaka Mitano Mpango kinaelezea tu tokea tulivyoanza kuzalisha ngozi mpaka tulipofeli, hamna mkakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna umuhimu na mimi nashauri kwamba, kwa kuwa tunataka kujenga viwanda kwanza tukubali kwamba viwanda ni matokeo, ni efficiency ya agro sector ni efficiency ya energy sector, ni efficiency ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Mheshimiwa Ndalichako, ni efficiency ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Mbarawa, ndiyo tunampata Waziri wa Viwanda na Biashara, Mheshimiwa Mwijage! There is no miracle, hakuna muujiza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ukienda pale Mkoa wa Tabora tunalima tumbaku na wakulima wa tumbaku wapo, wanafahamu utitiri wa kodi intermediaries wamejaa kati ya mkulima na mnunuzi kila intermediaries hapa anavuta kidogo mkulima anabaki maskini. Nimeona kwenye Mpango tunazungumzia special zones ambazo tutaweka either viwanda, sijaona Tabora, Tabora tunazalisha tumbaku haijatajwa, ningemwomba Mheshimiwa Dkt. Mpango na Dada yangu Mheshimiwa Ashatu... (Makofi)
MWENYEKITI: Mheshimiwa tunakushukuru kwa mchango wako mzuri, nilifanya makusudi kukuweka wa mwisho kwa jioni ya leo.