Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia, lakini niseme mimi pia ni Mjumbe katika Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira. Tumetoa ushauri kwenye taarifa yetu, lakini ni vema basi kuna mambo mengine ambayo tunaweza tukayazungumza angalau Wabunge wenzetu waweze kutuunga mkono katika Kamati yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ningependa kuanza na suala zima la mazingira. Kwa masikitiko makubwa niseme kwamba Ofisi hii ya Makamu wa Rais siku zote imekuwa ikipewa bajeti kidogo sana pamoja na kwamba Wizara ya Mazingira ni Wizara mtambuka, lakini bado Serikali imeendelea kuipa pesa kidogo Ofisi ya Makamu wa Rais ka upande wa Mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na udogo wa fedha hiyo, pamoja na udogo wa bajeti hiyo, bado fedha hii kupatikana kwake haipatikani kabisa. Tangu tulivyokutana mara ya mwisho na Ofisi ya Makamu wa Rais, mwezi Januari, kwa masikitiko makubwa mpaka leo tunavyozungumza hapa hawajawekewa hata shilingi moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama tunategemea mazingira ya nchi yetu ndiyo kila kitu katika ustawi wa nchi yetu, lakini bado katika Ofisi ya Mazingira bado fedha haiendi, watumishi pale wanashindwa kutekeleza majukumu yao kutokana na uwezo mdogo wa fedha walio nao. Wameishia watu wa NEMC, sasa hivi wanachokifanya fedha ambayo wanaitumia ni fedha ya kutoza faini kwa watu. Yaani sasa hivi imefika mahali wanapata fedha kwa ajili ya makosa ya watu, sasa sijui ni Serikali ya aina gani ambayo inaendeshwa kwa fedha ambazo ni makosa ya Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi hali ya mazingira nchini kwetu ni mbaya sana kuliko ambavyo tunaweza kuifikiria. Tumetembea kwenye maeneo mbalimbali, lakini baadhi ya miradi ambayo ilikuwa imepangiwa kwenye bajeti hii hatukuweza kufanikiwa kuiona kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Tumetembelea eneo moja tu ambalo tulikuwa kama vile tumeenda beach, tulipelekwa eneo la ufukwe la Ocean Road; ndilo eneo ambalo pekee tulipelekwa kama Kamati kwenda kuona sehemu ambayo wanategemea kujenga ukuta kwa ajili kuzuwia mmomonyoko ambao unakuja unasogea mpaka kufikia Ikulu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini maeneo mengine yote ambayo yalikuwa yamewekwa kwenye bajeti ya Serikali ya mwaka huu ya mazingira hakuna eneo lingine ambalo tumeweza kwenda zaidi ya maeneo ambayo Bunge lilitusaidia tumeweza kufika, kama Mwadui pamoja na Geita. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulipotembelea Mgodi wa Mwadui tulijionea hali halisi ya mazingira katika mgodi ule na kiukweli wanajitahidi kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kwamba maeneo ya mazingira katika mgodi ule yanalindwa pamoja na maeneo ya pembezoni ambayo wananchi wanaishi. Eneo la Mgodi wa Mwadui pamoja na wananchi wake wameweza kupewa elimu ya upandaji wa miti na jinsi ya kuvuna miti ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwadui walichowafundisha watu wanaoishi maeneo ya Kishapu ni kuhakikisha kwamba hawakati miti kama vile inavyofanyika maeneo mengine. Eneo lile wamefundishwa kukata miti kwa kukata matawi na kuacha shina liendelee ili ule mti uweze kuendelea kuwa mkubwa badala ya kukata mti mzima na kuacha kisiki na kutegemea kwamba watu waendelee kupanda miti mingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetembelea Mgodi wa Geita. Mgodi wa Geita kiukweli kwa kuhusiana na suala zima la maji machafu wamejitahidi kwa namna moja ama nyingine kuweza kuweka bwawa ambalo linahifadhi yale maji machafu. Lakini kwenye maeneo ya mazingira, hasa kwenye maeneo ya miti kwa kweli hawafanyi vizuri kwa sababu hali ni mbaya, wananchi wanakata miti sana, wananchi wanatengeneza mikaa kwa wingi kweli kweli! Kwa hiyo, tuliwashauri angalao kwenye maeneo ambayo yanawazunguka basi waweze kusaidia wale wananchi wa pale waweze kuwa wanapanda miti na kusaidia mazingira yaweze kuwa mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikwenda kwenye Mradi wa Ziwa Victoria. Huku ni masikitiko makubwa sana, kwasababu imefika mahali hali ya mazingira katika Mradi wa Ziwa Victoria kwa kweli si nzuri na hairidhishi. Tungemuomba sana Mheshimiwa Waziri atakapokuja kwenye majumuisho yake hebu ajaribu kutuambia katika huu Mradi wa Ziwa Victoria nini hasa kinachoendelea? Kwa sababu inavyoonekana kama Tanzania tunajitahidi kwa namna moja ama nyingine kuweza kuzuia hali ya mazingira ya Ziwa Victoria kuwa sawa, lakini ukiangalia nchi jirani ambazo zinatuzunguka na tulizoingianazo mkataba bado zenyewe hazitekelezi mkataba ule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima tufike mahali sasa na Watanzania tuangalie na nchi jirani za wenzetu ili yale ambayo tunakubaliana kwenye mikataba yetu yaweze kufanyiwa kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikizungumzia kuhusu suala zima la viwanda, sasa hivi viwanda vingi vya samaki Mwanza vinafungwa na vinafungwa kwa sababu ya ukosefu wa samaki katika Ziwa Victoria. Hali ni mbaya, kiwanda ambacho kilikuwa kinaweza kufanya kazi saa 24 leo wanaweza wakafanya kazi kwa shift mbili peke yake, ikizidi sana ni shift moja. Leo viwanda vya samaki vya Mwanza baadhi vimefungwa na baadhi vinaendelea kufanya kazi kwa kusuasua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ningependa kumshukuru Waziri wa Nishati na Madini kwa kukubali mapendekezo yetu na maoni yetu ya kumuomba waanze kununua transfoma zinazotengenezwa nchini kwetu. Kiwanda cha Tanelec kinatengeneza transfoma nzuri na Mheshimiwa Waziri pamoja na Kamati tumesikia wamesema kwamba, kuanzia sasa wataanza kununua transfoma kutoka nchini kwetu. Hilo ni suala zuri naomba nikupongeze Mheshimiwa Waziri na tufanye hivyo ili kuweza kuinua uchumi wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyotangulia kusema Mjumbe mwenzangu, Wizara ya Fedha imetengewa bajeti lakini mpaka leo tunavyozungumza tunakwenda karibu robo iliyobaki kumaliza bajeti, lakini fedha iliyokwenda ni only 7 point something billion. Jamani katika bilioni 42, bilioni saba kwenye Wizara ya Viwanda ni kitu gani ndugu zangu! Nafikiri hapa tunafanya masihara, tunaweza tukawa tunalaumu, lakini mwishowa siku Serikali; Mheshimiwa Mpango na Hazina yako hebu jaribuni kuangalia basi. Zile Wizara ambazo angalao mnasema kwamba zina kipaumbele hebu zisaidieni kuziwekea fedha ili waweze kutekeleza majukumu yao badala ya kukaa mnatusaundisha (mnatushawishi) kila siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kila wanapokuja watu wa Wizara ya Fedha ni habari ya kusaundishwa (kutushawishi) tu, lakini utekelezaji haupo. Ilifika mahali tuliwarudisha, tuliwafukuza na tukawaambia hatutakaa tusikilize taarifa yenu kwa sababu haina jipya. Kila wanapokuja wanakuja na yaleyale kumbe tatizo ni ukosefu wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wizara hii kuna kitu kinaitwa Fair Competition, hawa watu wanafanya kazi kubwa sana, yaani hawa watu ndio ambao wanazuia bidhaa fake kuingia nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Fair Competition wanafanya kazi ngumu lakini hawana watu ambao wanafanya kazi hizo. Leo Fair Competition kati ya wafanyakazi 125 wanaohitajika wana wafanyakazi 53 tu nchi nzima. Hebu fikiria mtegemee hawa watu waweze kufanya kazi nzuri, kazi hiyo wanaifanya kutokea wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Angellah Kairuki alituelea hapa kwamba, Ofisi yake ya Utumishi imeanza kuruhusu ajira; Mheshimiwa Angellah Kairuki, sijui ajira hizo zinakwenda upande gani? Kwa sababu kama kwenye Wizara mbalimbali hakuna watumishi ambao wanaajiriwa! Mheshimwia Waziri, hebu utatueleza ukweli, hawa watumishi mnawaajiri kwenye idara zipi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kusikitisha ni kwamba hawa watu wa FCC pia waafanya kazi nyingine ambazo ni za hatari sana, wanaingia bandarini wanakutana na watu, lakiniā€¦
(Hapa, kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante sana.