Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Bunge limekuwa kila siku moja ya ajenda yake ni kupata semina elekezi kupeleka kwa ma-RC pamoja na ma-DC. Lengo la hizi semina ni kwa sababu ya haya mambo yanayotokea, haya tunayoyasema kama hawa watu wangepatiwa semina elekezi wakajua mipaka ya mamlaka yao naamini yasingetokea. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, mercury ina tabia moja, ukiifukia chini ya ardhi hata kama ni kilometa tano chini ya ardhi, itapanda itaibuka juu. Sasa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ana tabia za mercury yaani ananyanyuka. Hali iliyopo sasa hivi ni kwamba yaani akitoka Rais anayefuatia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam yaani Waziri wa Mambo ya Ndani hayupo, IGP hayupo, Waziri Mkuu hayupo, hakuna mtu yeyote, Bunge kama mhimili halipo, yaani imefikia mahali…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ni vizuri nikali-clarify kidogo. Nafikiri Mheshimiwa Waziri hajaelewa au hajanisikia vizuri, hata akirudi kwenye Hansard ataona kitu ambacho nimekizungumza. Ninachokifanya hapa ni kutetea Baraza la Mawaziri pamoja na Waziri Mkuu, ndicho ninachokifanya hapa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, CCM kabla ya mwaka 2015 ndiyo chama kilichokuwa kinasifika kwa protocol, chama ambacho kilikuwa kinajua kiongozi gani afanye nini kwa wakati gani, suala la protocol lilikuwepo. Hata hivyo, sasa hivi protocol ile ambayo tulikuwa sisi wachanga wa vyama tunajifunza kwenu leo haipo kabisa, protocol imevurugika, hicho ndicho nilichokuwa nakielekea. Ndiyo maana nikasema ni kama vile, yaani mambo anayoyafanya ni kama vile anaona kama hakuna Waziri Mkuu, tena nimetumia neno ni kama. Wewe leo unakuta mtu ana-suspect mtu mmoja, huyohuyo ana-arrest, huyohuyo ana-interrogate, huyohuyo anahukumu just one person! Hakuna utaratibu huo katika nchi hii! Ndiyo maana ya hiki tunachokifanya hapa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nasema kitu kimoja, Rais anasikia, Wabunge tumelalamika kuhusu Tume leo ameteua Tume, anasikia. Rais akishauriwa vizuri mimi nina uhakika, akishauriwa vizuri kwa mawazo mtangamano akayasikiliza, atakuwa the best President lakini Rais akisikiliza mawazo ya upande mmoja hawezi kuwa Rais mzuri. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunachokifanya hapa tunataka Bunge kama mhimili ufanye kazi yake na tunataka Mawaziri wafanye kazi yao. Mimi niwapongeze, nakupongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa busara uliyoionesha, nakupongeza sana Waziri wa Mambo ya Ndani kwa busara uliyoionesha katika kipindi hiki, hii lazima tupongeze, nampongeza sana Kiongozi wa Upinzani pamoja na IGP kwa busara waliyoionesha. Wangekuwa hawana busara nina uhakika sasa hivi hili jambo lingekuwa limeshaharibu utaratibu wote wa nchi. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tunasema kwamba hatutaki mgongano wa haya mambo. Ndiyo maana tangu mwanzoni nikaelezea tabia ya mercury ukiidumbukiza hata kilometa tano itanyanyuka sasa hizi tabia ndiyo wanazo watu. Sisi tuliokwenda Jeshini kule tunafahamu zile 22 critics. Sasa tunachotaka wapelekeni na hawa vijana kule Jeshini wakajifunze, wapeni semina elekezi, kinyume na hapo mnaharibu. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wasanii, mmejadili kuhusu wasanii, tumewatumia kwenye kampeni za uchaguzi pande zote mbili, leo unawalipa wema kwa ubaya watu ambao wamezunguka nchi nzima kufanya kampeni kwenu. Wafanyabiashara waliochangia vyama vyetu vya kisiasa kwa ajili ya kushinda uchaguzi leo unawalipa wema kwa ubaya, hatuwezi kuendesha nchi katika huo mfumo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, misingi ya Taifa letu kama Tanzania au moja ya sifa kubwa ya Tanzania ni utu, kuheshimiana, busara, hekima na kusikilizana. Hayo ndiyo mambo ambayo tumekuwa tukiyahitaji, ndiyo misingi ya Utanzania. Kwa hiyo, tunachokifanya hapa siku zote tunataka muende mkamrekebishe Mkuu wa Mkoa asijigeuze yeye mamlaka zaidi ya Bunge…
Hatuwezi kukubaliana na jambo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.