Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia muda huu na mimi nichangie machache niliyonayo. Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza, jamani Waheshimiwa Wabunge sisi tumechaguliwa na wananchi kwa ajili ya kuwasaidia. Sasa basi tunaposhangilia hapa na tunapopitisha hivi vitu viwe kwa ajili ya maslahi ya wananchi. Kila Kamati iliyosimama hapa ilikuwa inalalamika kuhusu ufinyu wa bajeti. Bahati nzuri sasa hivi imeturudia sisi wenyewe na hii iwe fundisho kila kitu kinachokuja mnapitisha. Mimi ingekuwa amri yangu hizi meza zingekuwa za chuma ili kabla mtu hajapiga awe anafikiria maumivu. (Makofi/Kicheko) Mheshimiwa Mwenyekiti, kila Kamati imepewa bajeti ya shilingi milioni 10 kwa ajili ya safari za nje. Jamani hebu tujiulize Kamati ya chini kabisa ilikuwa na watu sio chini ya 18, hivi shilingi milioni 10 unaenda nchi gani, unatumia usafiri gani, bajaji? (Kicheko) Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, kitu ambacho nime-experience katika hizi Kamati kuwa Serikali inapokuja kujibu, inakuja timu ya watu 30 anayeongea ni mtu mmoja. Jamani huu ni ufujaji wa fedha hizi za wananchi kwani hamna kazi nyingine? Utakuta wanakuja wengi anajibu mtu mmoja, nusu saa halafu mistari yenyewe miwili wanaondoka, VX 8 zimekuja. Jamani huu ni ubadhirifu wa fedha za Watanzania. (Makofi/Kicheko) Mheshimiwa Mwenyekiti, suala langu la tatu ni kuhusu Wizara ya Mambo ya Nje, sasa hivi kila mkoa unaoenda unakutana na Wachina. Jamani hawa Wachina nawahakikishia tukianza kukutana nao labour ward haki ya Mungu nchi hii mwaka 2030 tunafanya sensa wao watakuwa wengi kuliko sisi. Kwa hiyo, Wizara ya Mambo ya Nje, naomba mliangalie suala hili. Wako Wachina wanaishi hawana passport hawajui viza ndio nini, wanaingia tu lakini sisi kwenda kwao wanatudhibiti. Kwa hiyo, naomba mliangalie suala hili. (Kicheko) Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Sheria Ndogo tulifanya ziara kwa Mpiga Chapa wa Serikali. Jamani Mawaziri, namwomba Rais aende katika Ofisi ya Mpiga Chapa wa Serikali, sijawahi kuona ofisi mbovu kama ile yaani ukienda huwezi ukategemea kama wanafanya kazi ya printing, haina tofauti na station ya TAZARA au ile station kubwa. Kwa hiyo, naomba Rais aende akatembelee pale, ina hali mbaya. Hawafanyi kazi yaani wakiletewa ku-print kazi ya Serikali wanaenda ku-print kwa Wahindi sasa siri za Serikali zinakuwa wapi tena? Siri si zinavuja huko mitaani halafu tunalalamika Serikali yetu haina siri. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la nne, jamani mimi Mlinga sipingi vita dhidi ya madawa ya kulevya. Ninacholalamika na kulaani ni mtu kutumia madaraka yake kupigana vita binafsi kuigeuza kuwa vita ya Kitaifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hicho ndicho ninachopinga. Mimi Mlinga niko tayari kusimama mbele ya Rais kumwambia chanzo cha vita hii. Kumwambia ukweli, vita haijaanza kwa ajili ya madawa ya kulevya, vita imeanza na ugomvi binafsi, baada ya kuona ita-backfire wakaigeuza kuwa vita ya madawa ya kulevya. Niko tayari kusimama mbele ya Rais achunguze chanzo ni nini? Wale wasanii waliowekwa ndani chanzo kilikuwa nini, haikuwa vita dhidi ya madawa ya kulevya. Niko tayari kusimama mbele yake kumwelezea aangalie ukurupukaji huu utatusababishia uvunjifu wa amani Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mmemtaja Gwajima ana watu, mmemtaja Mbowe wa CHADEMA watakaa pembeni, mtawataja akina Manji watu wa Yanga watakaa pembeni. Jamani uchungu wa mambo haya, kama una familia ukija kutajwa utayaona machungu yake, siyo rahisi hivyo mnavyofikiria. (Makofi/Kicheko) Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii umeniharibia heshima yangu mimi Mlinga na nina wananchi wangu kule Ulanga, nina mke wangu ana ndugu zake, nina watoto wangu wanasoma shule, hivi watoto wangu wanatembeaje huko walipo jamani. Leo hii nimekutaja wewe unahusika na madawa ya kulevya, hivi watu wanaonifahamu wanatembeaje huko waliko? Jamani haya mambo myasikie yasije yakawakuta. (Makofi/Kicheko) Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais amemteua IGP, Waziri wa Mambo ya Ndani, jamani mbona mko kimya, hamna shughuli za kufanya, kwa nini mnaachia watu wanadhalilishwa? Nchi yetu ina wakuu wa mikoa 25, nime-experience kinachoanzia Dar es Salaam Wakuu wa Mikoa wote wanafuata. Hivi kila Mkuu wa Mkoa akisimama akianza kufanya yale yanayofanyika Dar es Salaam jamani tutakuwa wapi? Kwa hiyo, tufikirie vitu kabla ya kufanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema sisi Wabunge siyo kwamba tunawaonea watu wivu.